Na. Peter Haule, WF, Dodoma.

Serikali imesema kuwa ina mpango wa kujenga vituo sita vya forodha mipakani katika mwaka wa fedha ujao wa 2025/26.

Hayo yalisema bungeni jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Hamad Hassan Chande (Mb), alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum, Mhe. Oliver Daniel Semuguruka, aliyetaka kujua mpango wa Serikali wa kuanza ujenzi wa Kituo cha Forodha katika Kijiji cha Mukikoro, Kata ya Mugoma - Ngara.

Mhe. Chande alisema kuwa Serikali imetenga jumla ya shilingi bilioni 1.1 ya ujenzi wa vituo Sita vya forodha kikiwemo kituo cha forodha Mugoma kilichopo Wilaya ya Ngara, mkoani Kagera mpakani mwa Tanzania na Burundi kwa mwaka ujao wa fedha.

Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Hamad Hassan Chande (Mb), akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum, Mhe. Oliver Daniel Semuguruka, aliyetaka kufahamu kuhusu mpango wa Serikali wa kuanza ujenzi wa Kituo cha Forodha katika Kijiji Mukikoro Kata ya Mugoma, Wilayani Ngara, mkoani Kagera, bungeni jijini Dodoma.


(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serilini, Wizara ya Fedha, Dodoma)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...