Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Bi. Zuhura Yunus amewasisitiza wafanyakazi wa sekta mbalimbali nchini kujenga tabia ya kushiriki michezo na mazoezi kwa ujumla ili kuimarisha afya zao na kuepuka magonjwa yasiyoyakuambukiza ambayo kwasasa ameeleza ni changamoto inayowakabili watu wengi ulimwenguni.
Bi. Zuhura ametoa wito huo wakati akifunga Bonanza la michezo (OSHA Bonanza) lililoandaliwa na kuratibiwa na Wakala wa Usalama na Afya Mahali pa Kazi (OSHA) kama sehemu ya maadhimisho ya Wiki ya Kimataifa ya Usalama na Afya Mahali Pa Kazi inayoadhimishwa kitaifa Mkoani Singida katika Viwanja vya Mandewa.
Bi. Zuhura ameeleza kuwa Serikali ya awamu ya sita chini ya uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan imekuwa ikihamasisha umuhimu wa michezo na mazoezi kwa wananchi katika kujenga afya na kupambana na magonjwa yasiyoyakuambukiza ikiwemo saratani, kisukari, magonjwa ya moyo na shindikizo la damu.
“Takwimu za Shirika la Afya Duniani (WHO) zinakadiria asilimia 75 ya vifo vyote vinavyotokea ulimwenguni kila mwaka husababishwa na magonjwa yasiyoyakuambukiza na hata Wizara ya Afya nichini inakadiria kati ya vifo 100 vinavyotokea kila mwaka vifo 33 vinasababishwa na magonjwa hayo, hivyo nawasishi wafanyakazi wote kuepuka mtindo mbaya wa maisha na kujenga tabia ya kufanya mazoezi ili kuepuka magonjwa haya” ameeleza Bi. Zuhura
Kwa upande wake Mtendaji Mkuu wa OSHA, Bi. Khadija Mwenda amesema madhumuni makubwa ya Bonanza hilo ni kutoa hamasa kwa wafanyakazi kushiriki michezo ili kujenga afya zao pamoja na kuimarisha uhusiano baina ya wafanyakazi huku akieleza kuwa taasisi yake itaendelea kulinda nguvu kazi kupitia programu mbalimbali ikiwemo kaguzi za usalama na afya ili kuhakikisha wafanyakazi wote wanakua salama na wenye afya njema ili watekeleze majukumu yao vyema.
Bonanza hilo lilijumuisha michezo mbalimbali ikiwemo mpira wa miguu,mpira wa pete, mbio za magunia, riadha, mbio za vijiti, kuvuta kamba, kukimbiza kuku,mchezo wa kukimbia na ndimu na katika michezo hiyo OSHA imetwaa ubingwa katika michezo mchezo ya mpira wa pete, riadha kwa wanawake na wanaume huku timu ya mpira wa miguu ya OSHA Sports Club ikiishia hatua ya nusu fainali katika mchezo wa mpira wa miguu.
Aidha, timu zilizoshiriki katika michezo mbalimbali ya Bonanza hilo lililofanyika katika viwanja vya VETA Singida ni timu kutoka OSHA, Wizara ya ujenzi, Mgodi wa Geita (GGM),Wizara ya Uchukuzu, Mahakama, Wizara ya Kilimo, Wizara ya Maji, Bohari ya Dawa (MSD),TANROADS,Shanta Gold Mine, Wizara ya Afya, Benki ya NMB, Ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikiali, Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) n.k.

Bi. Zuhura ametoa wito huo wakati akifunga Bonanza la michezo (OSHA Bonanza) lililoandaliwa na kuratibiwa na Wakala wa Usalama na Afya Mahali pa Kazi (OSHA) kama sehemu ya maadhimisho ya Wiki ya Kimataifa ya Usalama na Afya Mahali Pa Kazi inayoadhimishwa kitaifa Mkoani Singida katika Viwanja vya Mandewa.
Bi. Zuhura ameeleza kuwa Serikali ya awamu ya sita chini ya uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan imekuwa ikihamasisha umuhimu wa michezo na mazoezi kwa wananchi katika kujenga afya na kupambana na magonjwa yasiyoyakuambukiza ikiwemo saratani, kisukari, magonjwa ya moyo na shindikizo la damu.
“Takwimu za Shirika la Afya Duniani (WHO) zinakadiria asilimia 75 ya vifo vyote vinavyotokea ulimwenguni kila mwaka husababishwa na magonjwa yasiyoyakuambukiza na hata Wizara ya Afya nichini inakadiria kati ya vifo 100 vinavyotokea kila mwaka vifo 33 vinasababishwa na magonjwa hayo, hivyo nawasishi wafanyakazi wote kuepuka mtindo mbaya wa maisha na kujenga tabia ya kufanya mazoezi ili kuepuka magonjwa haya” ameeleza Bi. Zuhura
Kwa upande wake Mtendaji Mkuu wa OSHA, Bi. Khadija Mwenda amesema madhumuni makubwa ya Bonanza hilo ni kutoa hamasa kwa wafanyakazi kushiriki michezo ili kujenga afya zao pamoja na kuimarisha uhusiano baina ya wafanyakazi huku akieleza kuwa taasisi yake itaendelea kulinda nguvu kazi kupitia programu mbalimbali ikiwemo kaguzi za usalama na afya ili kuhakikisha wafanyakazi wote wanakua salama na wenye afya njema ili watekeleze majukumu yao vyema.
Bonanza hilo lilijumuisha michezo mbalimbali ikiwemo mpira wa miguu,mpira wa pete, mbio za magunia, riadha, mbio za vijiti, kuvuta kamba, kukimbiza kuku,mchezo wa kukimbia na ndimu na katika michezo hiyo OSHA imetwaa ubingwa katika michezo mchezo ya mpira wa pete, riadha kwa wanawake na wanaume huku timu ya mpira wa miguu ya OSHA Sports Club ikiishia hatua ya nusu fainali katika mchezo wa mpira wa miguu.
Aidha, timu zilizoshiriki katika michezo mbalimbali ya Bonanza hilo lililofanyika katika viwanja vya VETA Singida ni timu kutoka OSHA, Wizara ya ujenzi, Mgodi wa Geita (GGM),Wizara ya Uchukuzu, Mahakama, Wizara ya Kilimo, Wizara ya Maji, Bohari ya Dawa (MSD),TANROADS,Shanta Gold Mine, Wizara ya Afya, Benki ya NMB, Ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikiali, Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) n.k.

Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Bi. Zuhura Yunus akikabidhi zawadi ya kombe kwa kiongozi wa timu ya mpira wa pete ya OSHA, Rachel Nkoma. OSHA imetwaa ubingwa katika mpira wa pete baada ya kuifunga timu ya Wizara ya Maji magoli 17 kwa 14 katika mchezo wa fainali.
Mtendaji Mkuu wa OSHA, Bi. Khadija Mwenda akisisitiza umuhimu wa wafanyakazi kushiriki michezo wakati akizungumza na washiriki wa Bonanza la OSHA lililofanyika Mkoani Singida.
Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Bi. Zuhura Yunus akigawa zawadi ya vikombe na medali kwa washindi wa michezo mbalimbali katika Bonanza la OSHA lililofanyika katika Viwanja vya VETA Mkoani Singida.
Timu ya mpira wa pete ya OSHA ikicheza mchezo wa fainali dhidi ya timu ya Wizara ya Maji ambapo OSHA ilishinda goli 17 kwa 14 na kutwaa ubingwa wa Bonanza la OSHA kwa upende wa mchezo wa mpira wa pete.
Timu za wafanyakazi kutoka maeneo mbalimbali ya kazi nchini zikishiriki katika michezo tofauti tofauti katika Bonanza la OSHA lililofanyika katika Viwanja vya VETA Mkoani Singida.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...