MSAJILI wa Vyama vya Siasa Tanzania, Jaji Fransis Mutungi amewataka wananchi wawe makini na matumizi ya akili bandia au akili unde (AI), na habari za uongo ambazo zinalenga kusambaza propaganda na kupotosha umma.

Jaji Mutungi ameyasema hayo Mei 3, 2025 jijini Dar es Salaam katika kikao maalumu na wahariri wa vyombo mbalimbali vya habari kujadili masuala tofauti ikiwemo maandalizi ya Uchaguzi Mkuu.

“Ni vyema tukawa makini kipindi hiki hususan viongozi wa vyama vya siasa, tudumishe amani na mshikano kwani ndiyo msingi wa maendeleo, tuepuke na habari ambazo hatuna uhakika nazo hasa wakati huu katika matumizi ya teknolojia”Amesema

Jaji Mutungi amesema tukio la waraka feki wa Baraza la Maaskofu Tanzania (TEC), uliosambaa ni mfano halisi wa habari potofu na kwamba ni muhimu kutafuta habari katika vyama vya kuamini.

Hata hivyo amewataka viongozi wa vyama vya siasa kuwahimiza wananchi wakiwemo wanachama wao, kufuata sheria kudumisha amani na mshikamo hususan kipindi hiki cha kuelekea Uchaguzi Mkuu.

Aidha, amesema ni muhimu vijana na wanawake wanapata nafasi ya kushiriki mchakato wa uchaguzo iwe kwa kupiga kura kugombea au kushiriki midahalo, na kwamba vyombo vya habari vishiriki kutoa elimu hiyo.

Pamoja na hayo amesema wanaendelea kushirikiana na wadau mbalimbali wa uchaguzi ikiwemo Tume Huru ya Uchaguzi na ile ya Zanzibar, kuhakikisha wanazingatia maadili na kudumisha amani kufanikisha uchaguzi huru, haki na amani.















Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...