Na Janeth Raphael MichuziTv -Dodoma

Watendaji Wizara Wizara ya Kilimo watakiwa kuanza mchakato wa ununuzi wa ndege mpya tatu kwa ajili ya vituo vya Kilimo anga vya kanda vilivyopo katika mikoa ya Arusha,Mbeya na Mwanza lengo likiwa ni kudhibiti visumbufu vya mimea.

Waziri wa Kilimo Mhe. Hussein Bashe, ametoa maagizo hayo wakati wa hafla ya mapokezi ya ndege moja ya kudhibiti visumbufu vya mimea iliyonunuliwa na Serikali chini ya Wizara hiyo kwenye Kiwanja kidogo cha ndege Mkoani Dodoma ambayo itatumika katika kituo cha Kanda ya Kati.

“Vituo vyote hivi vinatakiwa viwe vina ndege na ‘drones’ kwa hiyo, mchakato wa kununua ndege tatu nyingine uanze sasa hivi. Ni lazima kama Nchi ijitegemee, dunia ya kubebana haipo. Lazima tuweze kutoa huduma, tumeshaanza kununua ‘drones’ za kufanya ‘survilence’, mwaka huu tunanunua drone kwa ajili ya ‘spraying’.” Mhe. Bashe.

Kadhalika, Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatilifu Tanzania (TPHPA) Prof. Joseph Ndunguru, amesema ndege hiyo inalenga kuleta mageuzi makubwa katika Sekta ya Kilimo kwa kuleta tija, ajira na kupanua masoko lakini pia kuimarisha hali ya chakula hapa nchini na kuongeza kuwa visumbufu vya mimea ni moja ya jitihada za Mamlaka katika kuleta tija kwenye sekta hiyo.

Hata hivyo, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe Rosemary Senyamule ameishukuru Wizara ya Kilimo kwa ununuzi wa Ndege hiyo ambayo italeta matumaini kwa Mkulima.

“Utashi huu unakwenda kuleta matumaini kwa Mkulima ambaye si mvivu, kwani amelima na kutunza mazao yake halafu mwishoni ndege anakula. Kwa Mkoa wa Dodoma itatuongezea upatikanaji wa chakula na wale wavivu sasa wataanza kulima kwani Dodoma pia tunapata athari ya Nzige maeneo ya Bahi na Kwelea kwelea maeneo ya Chemba, Kondoa na Kongwa.”

Ndege hiyo ‘Thrush 510 P2’ imegharimu TSh.  6,000,000,000 ina uwezo wa kukaa angani kwa zaidi ya saa 4 kutokana na tenki lake kubeba mafuta yenye ujazo wa lita 863, uwezo wa kubeba viuatilifu lita 1,930 uwezo wa kufanya udhibiti kwenye eneo la ekari 2400 kwa mara moja huku ikiwa na vifaa vya kisasa kwa ajili ya kutoa huduma  Kanda ya kati.





Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...