Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu-Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu- Mhe.Ridhiwani Kikwete, amesema Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, itaendelea kuimarisha Ustawi wa watu wasioona nchini, hususani katika upande wa elimu, afya miundombinu, ajira pamoja na ushiriki wao katika nafasi za kiuchumi kwenye jamii.

Mhe. Kikwete amebainisha kuwa serikali imeendelea kuimarisha ustawi wa watu wa wasioonakwa kuwapatia fursa za kuajiriwa, ujumuishwaji katika masuala ya TEHAMA, uboreshaji wa miundombinu ya elimu, uwezeshaji kupitia mikopo ya wajasiriamali na upatikanaji wa vifaa saidizi.

Ameyasema hayo alipokutana na kufanya mazungumzo na wajumbe wa Halmashauri kuu ya Chama cha wasioona Tanzania (TLB) ofisini kwake jijini Dodoma.

Amesisitiza kuwa serikali tayari inao Mkakati wa teknolojia Saidizi na Mfumo wa kielektroniki wa Taarifa na Kanzidata ya Watu wenye Ulemavu (PD-MIS) ambao unasaidia Serikali kupanga mipango ya huduma wezeshi kwa watu Wenye Ulemavu nchini wakiwemo watu wasiiona.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa TLB mkoani Shinyanga Marco Mashauri, ameishukuru serikali kwa kuendelea kuboresha ustawi wao kupitia TLB ambalo ni jukwaa la wasioona linalowawezesha kukutana, kuweza kujieleza,kuielimisha jamii juu ya uwezo wao, na mahitaji yao katika nyanja zote za maisha.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...