MWENYEKITI wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Mary Chatanda, amewasihi wananchi hususan wanawake kujitokeza kwa wingi katika uchsguzi mkuu wa Oktoba mwaka huu.


Amesema ni haki ya Kila mtanzania kushiriki katika uchaguzi huo na kuwachagua Viongozi watakaochagiza juhudi za maendeleo zinazofanywa na serikari chini ya Rais Dk.Samia Suluhu Hassan, kuwaletea maendeleo.

Chatanda ameyasema hayo wlayani Mkuranga, mkoani Pwani katika ziara yake ya kukagua utekelezaji wa Ilani ya CCM.

Katika ziara hiyo ameambatana na 
Makamu Mwenyekiti wa UWT Zainab Khamis Shomari na Wajumbe wa Kamati Tendaji wa umoja huo na Wajumbe wa Baraza Kuu la UWT.

Amesema Rais Dk Samia , ametoa fedha nyingi za maendeleo mkoani humo, hivyo ziara hiyo ililenga kujiridhisha na maendeleo yaliyofanywa.

Pia kuielezea Ilani mpya ya CCM kwa 2025/2030 kwa wananchi hivyo kuwasihi kujitokeza kupiga kura Oktoba ili kuwachagua Viongozi sahihi katika maeneo yao.

Akitoa salamu kwa Mwenyekiti wa UWT, Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga Khadija Nasri, amesema kwa asilimia kubwa miradi iliyoanishwa kwenye Ilani ya CCM imetekelezwa kikamilifu hivyo wana kila sababu ya kumshukuru. Rais Dk. Sami.

Jumla ya miradi 39 yenye thamani ya zaidi ya sh. bilioni 500 imetekelezwa na kukaguliwa na viongozi hao WA UWT wilayani humo.



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...