MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango ametembelea Kampuni ya Kimataifa ya Uzalishaji Vifaa Tiba ya Health 3000 iliyopo Roma nchini Italia leo tarehe 23 Juni 2025.
Makamu wa Rais amefanya mazungumzo na viongozi wa kampuni hiyo wakiongozwa na Mwenyekiti wa Kampuni hiyo Maurizio Flammini pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni hiyo Bi.Eleonora Flammini. Mazungumzo hayo yamelenga ushirikiano baina ya Tanzania na Kampuni ya Health 3000 hususani katika matibabu kwa njia ya mtandao (Telemedicine).
Kampuni hiyo ni moja ya Makampuni yaliyo chini ya mwamvuli wa FG Group ambayo imejikita katika kutoa huduma za afya hususani uzalishaji wa vifaa tiba kwa kutumia teknolojia za kisasa.
Makamu wa Rais yupo nchini Italia kumwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika Mkutano wa Ubia wa Maendeleo kati ya Afrika na Serikali ya Italia (Mattei Plan) pamoja na mikutano mbalimbali ya uwili.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango akishuhudia matumizi ya teknolojia katika matibabu kwa njia ya mtandao wakati alipotembelea Kampuni ya Kimataifa ya Uzalishaji Vifaa Tiba ya Health 3000 iliyopo Roma nchini Italia leo tarehe 23 Juni 2025.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango akisalimiana na Mwenyekiti wa Kampuni ya Kimataifa ya Uzalishaji Vifaa Tiba ya Health 3000 Maurizio Flammini wakati akiwasili katika Makao Makuu ya Kampuni hiyo Roma nchini Italia leo tarehe 23 Juni 2025.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango akifanya mazungumzo na Viongozi wa Kampuni ya Kimataifa ya Uzalishaji Vifaa Tiba ya Health 3000 wakiongozwa na Mwenyekiti wa Kampuni hiyo Maurizio Flammini kuhusu matibabu kwa njia ya mtandao (Telemedicine). Mazungumzo hayo yamefanyika katika Makao Makuu ya Kampuni Roma nchini Italia leo tarehe 23 Juni 2025.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...