Na Emmanuel Mbatilo, Michuzi Tv
SERIKALI imeendelea kuliimarisha jeshi la polisi kwa kuboresha mazingira ya kazi na kuongeza miundombinu, ambapo vituo vya polisi 472 vimejengwa hadi ngazi ya kata na shehia.
Ameyasema hayo leo Juni 27, 2025 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan wakati akitoa hotuba ya kuhitimisha shughuli za Bunge la 12 Jijini Dodoma.
"Tumeboresha makazi ya askari na kununua vitendea kazi, ikiwemo magari na pikipiki, kwa ajili ya kazi za utawala na operesheni. Aidha, askari wapya 16,009 wameajiriwa, huku Maofisa,Wakaguzi na Askari 10,363 wakipandishwa vyeo". Amesema Rais Samia
Aidha ametoa pongezi kwa Jeshi la Polisi kwa kazi kubwa na nzuri wanayoifanya kwa kuzuia uhalifu.
"Kasi ya kuwabaini na kuwakamata wahalifu, na kuwafikisha Mahakamani imeongezeka. Jambo ambalo bado hatujafanikiwa vya kutosha ni ajali za barabarani. Lazima nazo tuendelee kuzitafutia muarobaini wake.
Pamoja na hayo Rais Samia amelielekeza Jeshi la Polisi kuongeza jitihada katika kukomesha matukio ya watu kupotea.















SERIKALI imeendelea kuliimarisha jeshi la polisi kwa kuboresha mazingira ya kazi na kuongeza miundombinu, ambapo vituo vya polisi 472 vimejengwa hadi ngazi ya kata na shehia.
Ameyasema hayo leo Juni 27, 2025 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan wakati akitoa hotuba ya kuhitimisha shughuli za Bunge la 12 Jijini Dodoma.
"Tumeboresha makazi ya askari na kununua vitendea kazi, ikiwemo magari na pikipiki, kwa ajili ya kazi za utawala na operesheni. Aidha, askari wapya 16,009 wameajiriwa, huku Maofisa,Wakaguzi na Askari 10,363 wakipandishwa vyeo". Amesema Rais Samia
Aidha ametoa pongezi kwa Jeshi la Polisi kwa kazi kubwa na nzuri wanayoifanya kwa kuzuia uhalifu.
"Kasi ya kuwabaini na kuwakamata wahalifu, na kuwafikisha Mahakamani imeongezeka. Jambo ambalo bado hatujafanikiwa vya kutosha ni ajali za barabarani. Lazima nazo tuendelee kuzitafutia muarobaini wake.
Pamoja na hayo Rais Samia amelielekeza Jeshi la Polisi kuongeza jitihada katika kukomesha matukio ya watu kupotea.
















Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...