Kupitia anwani ya www.tausi.tamisemi.go.tz, wafanyabiashara wataweza kuona maeneo yote ya biashara yaliyotangazwa kwa njia ya mnada. Mnada huu wa kielektroniki utafanyika kuanzia tarehe 05 Juni, 2025 saa 1:00 Asubuhi hadi tarehe 11 Juni, 2025 saa 1:00 Asubuhi.
Ili kushiriki, mfanyabiashara anapaswa kujisajili kwenye mfumo wa TAUSI PORTAL akiwa na taarifa zifuatazo:
Namba ya Kitambulisho cha Taifa (NIDA)
Namba ya Mlipa Kodi (TIN)
Barua pepe (Email)
Namba ya simu
Wananchi na wafanyabiashara wote mnaombwa kutumia fursa hii muhimu kwa ushiriki wa haki na uwazi.
Imetolewa na:
Ashraph Y. Abdulkarim
MENEJA MKUU
Shirika la Masoko ya Kariakoo
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...