Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi akizungumza na kuagana na Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Philip Isdory Mpango, baada ya kumalizika kwa Mkutano Mkuu Maalum wa CCM Taifa.
Mkutano huo ulioongozwa na Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan, ulifanyika kwa njia ya mtandao katika Ukumbi wa Mikutano wa NEC, Makao Makuu ya CCM, Jumamosi tarehe 26 Julai 2025, jijini Dodoma.
Wengine pichani, ni Wajumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, ambao ni, Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Dotto Biteko (kulia) pamoja na Spika wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar, Mhe Zubeir Ali Maulid.






Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...