Afisa Rasilimali Watu Mwandamizi kutoka Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira ( NEMC) Bi. Shukrani J. Haule amekabidhiwa tuzo ya Mfanyakazi Hodari wa Taasisi katika Mkutano wa Jumuiya za Wataalam wa Usimamizi wa Rasilimali Watu na Utawala katika Utumishi wa Umma Tanzania (TAPA-HR), unaofanyika Jijini Arusha Katika Ukumbi wa kituo cha Mikutano cha kimataifa (AICC).

Bi. Shukrani amekabidhiwa tuzo hiyo leo 23 Julai,2025 na Katibu Mkuu Kiongozi wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Mhandisi Zena Ahmed Said.

Mkutano huu umewakutanisha wataalam zaidi ya 900 kutoka Wakala wa Serikali, Taasisi za Umma, Wizara, Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa ambao wanasimamia Rasilimali Watu na Utawala.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...