Wataalam wa Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC), Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA),Wizara ya Mifugo na Uvuvi,Wizara ya Uchukuzi ,Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Lindi pamoja na Halmshauri ya Wilaya ya Kilwa wakitembelea mradi wa Ujenzi wa Bandari ya Uvuvi Kilwa Mkoani Lindi
Wataalamu wa Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC), Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA),Wizara ya Mifugo na Uvuvi,Wizara ya Uchukuzi ,Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Lindi pamoja na Halmshauri ya Wilaya ya Kilwa.


*TASAC yajiandaa katika kutoa mafunzo mbalimbali mara baada ya kuanza bandari hiyo

Na Mwandishi Wetu ,Kilwa
WATAALAM wa Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC), Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA),Wizara ya Mifugo na Uvuvi,Wizara ya Uchukuzi ,Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Lindi pamoja na Halmshauri ya Wilaya ya Kilwa wameunda kamati ndogo ya kutafuta mbinu bora ya uendeshaji wa Bandari ya Uvuvi Kilwa mara baada ya kukamilika.

Kikao hicho kimefanyika baada ya ujenzi Bandari hiyo kufikia asilimia 82 ili mara baada ya kukamilika uende sambamba na uendeshaji.

Akizungumza katika ziara iliyoandaliwa na Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC) ya kutembelea Bandari ya Kilwa , Mkurugenzi wa Huduma za Uchukuzi Wizara ya Uchukuzi Biseko Chiganga amesema timu hiyo ya wataalamu ikikamilisha kazi yake itatoa muelekeo ya namna ya uendeshaji wa bandari na kupeleka ngazi za juu.

Biseko amesema timu hiyo ya wataalamu, imejumuisha wataalamu katika kuwa na mipango ya kufanya Bandari hiyo kusimamia katika viwango vya Kimataifa katika uendeshaji wa Bandari ya Uvuvi.

"Tumefanya ziara katika mradi na kufanya kikao cha pamoja kuangalia kabla ya mradi kukamilika tuangalie changamoto zilizopo na namna ya kuendesha bandari hii kwa ngazi ya wataalamu, kwani yapo mambo ya kitaalamu kwa ngazi ya awali, hizi kamati za kitaalamu zikikamilisha kazi yake ndio utatoa mwelekeo wa uendeshaji wa bandari,"amesema.

Kwa upande wake Mkurugenzi Udhibiti na Usimamizi wa Huduma za Usafiri Majini Nelson Mlali amesema wametembelea kujionea ujenzi wa bandari hiyo ili kujipanga namna ya uendeshaji wake mradi utakapokamilika.

"Sisi TASAC ni wadhibiti wa usafiri wa njia ya maji tumewaeleza wadau na majukumu yetu mradi utakapokamilika, mradi huu ukikamilika unakuwa bandari na bandari na bandari ni moja ya wadau unaodhibiti huduma zake kwa hiyo tumeeleza namna ambavyo tutaisimamia bandari hii,"amesema Mlali

Mlali amesema miongoni mwa majukumu yao bandari hiyo ikikamilika ni kuwapa elimu mabaharia watakaoendesha huduma za meli za uvuvi,usimamizi wa mawakala wa meli,forodha pamoja na kampuni ndogo ndogo za kusimamia huduma za vyakula.

Akizungumzia manufaa ya mradi huo, Jackson Ally mkazi wa Kilwa Masoko amesema vijana watakuza uchumi kutokana shughuli zitazokuwepo katika Bandari hiyo.

"Bandari hii kwetu tunaiona kama faraja yetu, mazao ya uvuvi yataongezeka kwasababu uvuvi utakuwa wa kisasa,tutapata ajira na vijana wengi wataondoka vijiweni na kuchangamkia fursa "amesema.


Wataalamu wa Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC), Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA),Wizara ya Mifugo na Uvuvi,Wizara ya Uchukuzi ,Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Lindi pamoja na Halmshauri ya Wilaya ya Kilwa wakipeana maelezo kuhusiana na ujenzi wa Bandari ya Uvuvi Kilwa mkoani Lindi.
Muonekano wa Jengo la Utawala la Bandari ya Uvuvi Kilwa ,mkoani Lindi
Muonekano wa Jengo la Bandari ya Uvuvi Kilwa sehemu za uendeshaji  ,mkoani Lindi
Wataalamu wa Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC), Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA),Wizara ya Mifugo na Uvuvi,Wizara ya Uchukuzi ,Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Lindi pamoja na Halmshauri ya Wilaya ya Kilwa wakiwa  katika picha ya pamoja mara baada ya kutembelea ujenzi wa Bandari ya Uvuvi Kilwa mkoani Lindi.
Mkurugenzi wa Huduma za Uchukuzi Wizara ya Uchukuzi Biseko Chiganga akizungumza na waandishi kuhusiana  ziara ya kutembelea mradi huo namna utavyoendeshwa kitaalam kwa viwango vya kimataifa vya uendeshaji wa bandari ya uvuvi nchini.

Mkurugenzi Udhibiti na Usimamizi wa Huduma za Usafiri Majini Nelson Mlali  akizungumza kuhusiana na TASAC katika shughuli zitazofanyika mara baada ya Bandari ya Uvuvi  itapoanza kufanya kazi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...