Na Pamela Mollel,Arusha


Mkoa wa Arusha umepongezwa kwa kufanya vizuri katika utekelezaji wa Agenda ya Taifa ya Kuwekeza katika Afya na Maendeleo ya Vijana Balehe.

Timu ya tathmini kutoka Ofisi ya Rais – TAMISEMI na Wizara ya Maendeleo ya Jamii ilikutana Agosti 11, 2025 kwenye ukumbi mpya wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha na kubaini kuwa juhudi za mkoa huo zinaendelea kuzaa matunda.

Mafanikio yaliyoangaziwa ni pamoja na elimu ya afya ya uzazi kwa vijana, huduma rafiki kwenye vituo vya afya, ushirikishwaji wa vijana katika maamuzi, pamoja na mikakati ya kujenga stadi za maisha na ujasiriamali.

Mmoja wa wajumbe wa tathmini alisema:

“Arusha ni mfano wa kuigwa. Ushirikiano wa serikali, jamii na wadau umeleta matokeo chanya kwa vijana.”

Uwekezaji huu unatajwa kuwa msingi muhimu kwa maendeleo ya vijana na mustakabali wa taifa.



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...