Na Pamela Mollel,Arusha

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mhe. Kenani Laban Kihongosi, ametoa wito kwa wananchi wa Arusha na wageni mbalimbali kujitokeza kwa wingi kushiriki na kutumia fursa zinazopatikana kupitia mashindano ya Meru Forest Adventure Race 2025.

Akizindua msimu wa tatu wa mashindano hayo yanayotarajiwa kufanyika katika hifadhi ya Napuru, eneo la utalii wa ikolojia nje kidogo ya Jiji la Arusha, Mhe. Kihongosi amesema matukio kama hayo yamekuwa na mchango mkubwa katika kusisimua uchumi wa wananchi mmoja mmoja pamoja na uchumi wa Mkoa wa Arusha kwa ujumla.

“Tunapopokea wageni kuna fursa nyingi za kiuchumi tunapata. Wageni watalala kwenye hoteli zetu, wenye hoteli watapata kipato, wafanyabiashara watauza mboga na vyakula, maana yake ni fursa kwa wananchi wengi ndani ya Mkoa wetu kwani hata magari yatasafirisha watu pia na hivyo kuwa fursa ya kiuchumi kwa wasafirishaji,” amesema Kihongosi.

Kwa upande wake, Mhifadhi Mkuu wa Msitu wa Meru/Usa (Meru Forest), Bw. Ali Maggid, amesema mashindano hayo yameendelea kukua mwaka hadi mwaka ambapo msimu wa kwanza yalihusisha washiriki 300, msimu wa pili washiriki 500 na kwa mwaka huu makadirio ni zaidi ya washiriki 700.

Ameongeza kuwa maandalizi yanaendelea vizuri huku burudani, mbio nyingine na zawadi mbalimbali zikiwa zimeongezwa ili kuvutia washiriki wengi zaidi.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...