Tanzania na Japan zimekubaliana kuimarisha ushirikiano katika sekta za biashara, uwekezaji, uendelezaji rasilimali watu, miradi mikubwa ya maendeleo na miradi ya msingi (Grassroots projects), na kilimo ikiwemo ukuzaji wa uzalishaji wa mazao ya kahawa, pamba na korosho.
Hayo yamebainishwa wakati wa kikao kati ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mheshimiwa Balozi Mahmoud Thabit Kombo (Mb.) na Waziri wa Mambo ya Nje wa Japan, Mheshimiwa Takeshi Iwaya kilichofanyika pembezoni mwa Mkutano wa TICAD 9 jijini Yokohama Agosti 21, 2025.
Viongozi hao pia wameahidi kuendelea kushirikiana katika masuala ya kimataifa, hususan kwenye agenda zenye manufaa kwa pande zote na utekelezaji wa miradi ya kimkakati kwa njia ya ubia wa sekta ya umma na binafsi.



Hayo yamebainishwa wakati wa kikao kati ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mheshimiwa Balozi Mahmoud Thabit Kombo (Mb.) na Waziri wa Mambo ya Nje wa Japan, Mheshimiwa Takeshi Iwaya kilichofanyika pembezoni mwa Mkutano wa TICAD 9 jijini Yokohama Agosti 21, 2025.
Viongozi hao pia wameahidi kuendelea kushirikiana katika masuala ya kimataifa, hususan kwenye agenda zenye manufaa kwa pande zote na utekelezaji wa miradi ya kimkakati kwa njia ya ubia wa sekta ya umma na binafsi.




Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...