MGOMBEA Mwenza wa Urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi, amesema chama hicho kikipewa ridhaa ya kuongoza katika kipindi cha miaka mitano ijayo, kitahakikisha changamoto ya maji katika Wilaya ya Ilala na Jimbo la Segerea inabaki kuwa historia.
Amesema azma ya CCM ni kuanzisha mradi mkubwa wa uzalishaji na usambazaji maji kwa maeneo hayo, sambamba na kupanua mtandao wa mabomba ili kufikisha huduma kila sehemu.
Aidha, mabomba yaliyoharibika au kukatika chini ya ardhi yatafukuliwa na kuwekwa mapya ili kuboresha upatikanaji wa maji safi na salama.
Dk. Nchimbi ameongeza kuwa Serikali ya CCM itajenga tanki kubwa la maji kwa ajili ya Jimbo la Segerea, ambapo kwa sasa lina ujazo wa mita za mraba 273 pekee, lakini litaboreshwa na kuongezwa mara nne hadi kufikia ujazo wa mita za mraba 845 milioni.
Akizungumza katika mkutano wa kampeni za CCM uliofanyika Jimbo la Segerea, Wilaya ya Ilala mkoani Dar es Salaam, Dk. Nchimbi alisema hatua hiyo inalenga kutatua kero kubwa inayowakabili wakazi wa maeneo hayo kwa muda mrefu.
Pamoja na mambo mengine,Dkt.Nchimbi alipata nafasi ya kuwanadi Wagombea Ubunge wa mkoa huo,akiwemo Mgombea Ubunge wa Jimbo la Segerea,Ndugu Bonnah Kamoli pamoja na Madiwani











Amesema azma ya CCM ni kuanzisha mradi mkubwa wa uzalishaji na usambazaji maji kwa maeneo hayo, sambamba na kupanua mtandao wa mabomba ili kufikisha huduma kila sehemu.
Aidha, mabomba yaliyoharibika au kukatika chini ya ardhi yatafukuliwa na kuwekwa mapya ili kuboresha upatikanaji wa maji safi na salama.
Dk. Nchimbi ameongeza kuwa Serikali ya CCM itajenga tanki kubwa la maji kwa ajili ya Jimbo la Segerea, ambapo kwa sasa lina ujazo wa mita za mraba 273 pekee, lakini litaboreshwa na kuongezwa mara nne hadi kufikia ujazo wa mita za mraba 845 milioni.
Akizungumza katika mkutano wa kampeni za CCM uliofanyika Jimbo la Segerea, Wilaya ya Ilala mkoani Dar es Salaam, Dk. Nchimbi alisema hatua hiyo inalenga kutatua kero kubwa inayowakabili wakazi wa maeneo hayo kwa muda mrefu.
Pamoja na mambo mengine,Dkt.Nchimbi alipata nafasi ya kuwanadi Wagombea Ubunge wa mkoa huo,akiwemo Mgombea Ubunge wa Jimbo la Segerea,Ndugu Bonnah Kamoli pamoja na Madiwani












Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...