Kikao cha 19 cha Kamati ya Mifuko na Programu za Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi kimefanyika Mkoani Arusha katika ukumbi wa VETA-Njiro kikihusisha wajumbe kutoka taasisi mbalimbali.
Kikao hicho kimekusudia kujadili maendeleo ya mifuko na programu za uwezeshaji hapa nchini ikiwemo mifuko inayotoa mikopo, dhamana, ruzuku pamoja na programu mbalimbali za uwezeshaji wananchi kiuchumi.
Washiriki wa kikao hiki ni wajumbe wote wa kamati hiyo, waratibu wa mifuko na programu za uwezeshaji pamoja na wataalam wa TEHAMA.
Katika kikao hicho, wajumbe walipata pia fursa ya kuona Mfumo Jumuishi wa Utekelezaji wa Sera ya Taifa ya Uwezeshaji (National Empowerment Management Information System – NEMIS).




























Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...