Mgombea wa nafasi ya udiwani kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika Kata ya Ng’apa , Jimbo la Lindi Mjini Ndugu Issa Ngasha amewaomba wananchi wa kata hiyo kuiamini CCM na kuakikisha wanajitokeza kupiga kura katika uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 29, 2025.
Akizungumza na wananchi wa kata ya Ng’apa katika uzinduzi rasmi wa kampeni uliofanyika tarehe 29 Septemba 2025.
Ngasha amesema wananchi wanapaswa kujitokeza kuchagua viongozi Kwani ni haki yao kikatiba na endapo yeye atachaguliwa na wananchi wa kata ya Ng’apa ataitumia nafasi hiyo kwa kufanya kazi kikamilifu katika kuhakikisha anatatua changamoto za wananchi.
Pia Ngasha amewaomba wananchi wa kata hiyo Kumchagua Dkt Samia Suluhu Hassan ,Mbunge wa Jimbo la Lindi Mjini Mohammed Utaly ili waweze kuleta maendeleo.
Uzinduzi huo uliambatana na shamrashamra na hamasa kubwa kutoka kwa wanachaman wa CCM na wakazi wa kata hiyo, mgeni rasmi akiwa ni Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM Wilaya ya Lindi Mjini , Jamadin Mandoa ambaye , aliwasihi wananchi kumuunga mkono Ngasha kwa kuwa ni kiongozi mwenye maono, uaminifu, na uzoefu wa kutosha.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...