Na Oscar Assenga,TANGA.
IKIWA zimesali siku chache kuingia kwenye uchaguzi Mkuu Octoba 29 Ofisi ya Vyama vya Msajili nchini imekutana naviongozi wa vyama vya siasa mkoani Tanga kwa lengo la kutoa elimu ya masuala mbalimbali yanayohusu uchaguzi kuhakikisha vinafuata sheria na kanuni zilizowekwa.
Elimu hiyo ilifanyika leo kwenye Ukumbi wa Halmashauri ya Jiji la Tanga ikishirikisha viongozi kutoka wilaya za Tanga,Pangani na Muheza.
Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo, Afisa kutoka Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa nchini Edna Assey alisema wameona ni vema katika kipindi cha uchaguzi kusiwe na makandokando kuwa na ustaarabu kwa maana kufuata sheria,kanuni zilizowekwa kwa ofisi ya msajili wa vyama vya siasa na Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi.
Alisema waliona ni muhimu kukutana na viongozi wa ngazi za wilaya kutokana na kwamba ndio wanasimamisha wagombea ngazi ya kata na wabunge katika maeneo mbalimbali hivyo wanahaki ya kupatiwa elimu hiyo.
“Katika kutoa elimu hii ni kukumbusha sheria zilizopo katika ofisi ya msajili ,sheria ya vyama vyas siasa sura namba namba 257 sheria ya gharama za uchaguzi sura namba 278 sheria hii ndio ambayo zinaiweka vyama vya siasa katika uchaguzi “Alisema
Aidha alisema katika sheria hizo kuna maeneo au vitendo haviruhusiwi kufanywa wakati wa uchaguzi na ndio ilikuwa agenda kuu ya hayo mafunzo na waliona ni muhimu kuwakumbusha na kuwaelimisha wao kama viongozi wanapokwenda kwenye ngazi za kwa wagombea,mawakala,viongozi na timu za kampeni kuwaelewisha kuna makatazo hayo yamefanyika kwenye sheria .
“Tunawaomba mfanye kampeni za kistaarabu,ofisi ya Msajili inawataka kufanya kazi kama chama ,kama taasisi na elimu hii iwafikie walengwa tunategemea itakuwa hivyo hivyo lakini nawasihi kama kuna malalamiko tuyapeleke kwenye kamati za maadili lakini mambo ya kurusha kwenye mitandao ya kijamii sio nzuri”Alisema
Hata hivyo alisisitiza iwapo wataona kuna eneo ambalo lina changamoto ni vema wawandikie au wapeleke kwa msimamizi wa uchaguzi au kamati ya maadili huku akitoa wito wahakikisha jambo hilo linakuwa na ukweli kwa maana sheria inakataza kutoa taarifa za uongo.
Katika hatua nyengine Ofisa Msajili huyo alisema kwamba vyama vya siasa vimekatazwa kunadi sera zinazopingana na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Katiba ya Zanzibar pamoja na Sheria zingine za nchi hasa katika kipindi hiki kuelekea katika uchaguzi mkuu wa Urais,Wabunge na Madiwani.
Alisema kwamba vyama hicho vimekatazwa kuunda vikundi vya ulinzi na usalama vya aina yoyote au kuwa na taasisi inayolenga kufanya majukumu ya Jeshi la Polisi lakini vikosi vingine vya ulinzi na usalama wa nchi.
Awali akizungumza Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Tanga Bahati Kahindi alisema kwamba katika semina hiyo watapitishwa kwenye gharama za uchaguzi na mambo ya maadili na kampeni ambayo ni mambo muhimu kuelekea kwenye uchaguzi huo.
Awali akizungumza Mwenyekiti wa UDP Mkoa wa Tanga Peter Mhina alishukuru kwa mafunzo hayo huku akishauri ni vyema vyama vya siasa kuwezesha kuanzia Rais, Wabunge na Madiwani ili waweze kufikia maeneo mengi na kuzungumza na wananchi kunadi sera.
“Tunaomba tume ituangalie wao wa vyama vya upinzani kwa sababu wote wapo kwenye sheria ya vyama vya siasa na sio chama tawala pekee maana nchi ni ya vyama vingi”Alisema
Hata hivyo kwa upande wake Katibu wa CCM wilaya ya Tanga Jamali Kimji alishukuru kwa kupatiwa elimu na ofisi ya msajili ambapo alisema ni elimu nzuri kwa sababu wamezungumza sheria katika tararibu zote za gharama za fedha kwa mgombea.
Alisema pia sheria hiyo katika mikutano na mambo mengine ambayo ni jambo nzuri na kampeni zimeshaanza kwa maana vipi vitu wameviona wengine wanafanya bila kujua kuwape elimu ni jambo nzuri na itasaidia kampeni zao kwenda vizuri.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...