Na Pamela Mollel,Arusha
Tanzania inaendelea kupiga hatua kubwa katika sekta ya fedha ambapo kijana mwekezaji wa kike, Mishel Mrema, amepongeza jitihada za Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kupigania ndoto za vijana wa Kitanzania na kutoa fursa za kufanya uwekezaji bila ubaguzi.
Alisema anamshukuru Rais Samia kwa kupambania vijana katika kipindi chake cha urais kwa kunyanyua vijana.
Mrema aliongeza kuwa Rais ameweza kuinua vijana kupitia nyanja mbalimbali ikiwemo kilimo, utalii, uchumi na huduma za kifedha kama Bureau de Change. Pia alibainisha kuwa kupitia Royal Tour, wageni kutoka mataifa mbalimbali wamefanikisha fursa nyingi za huduma za kifedha nchini.
Aidha, alitoa wito kwa wananchi pamoja na wageni kutembelea taasisi hiyo ili kubadilishana fedha jijini Arusha, akibainisha kuwa Serene Safari Bureau de Change inalenga kutoa huduma bora za ubadilishaji fedha za kigeni sambamba na kusaidia vijana kupata ajira.
VIONGOZI WAPONGEZA HATUA HIYO
Mgeni rasmi katika hafla ya uzinduzi huo jijini Septemba 27,2025, Iris Naushad Makere, Kamishna wa Mkoa wa Tanzania Girl Guides, alisema kuwa maadili, bidii na roho ya kujituma vimekuwa dira ya maendeleo ya taasisi hiyo. Aliongeza kuwa kuanzishwa kwa taasisi ya kifedha kama Serene Safari Bureau de Change ni ubunifu wenye mchango mkubwa katika kukuza uchumi wa taifa la Tanzania.
Kwa upande wake, Hashim Chamani, Mkurugenzi wa Furaha Safari Bureau de Change, alieleza furaha yake kwa ujio wa taasisi hiyo mpya akisisitiza kuwa itaongeza ushindani wa kibiashara, kuboresha huduma za kifedha na kuchangia ajira kwa vijana. Chamani pia alimpongeza Rais Samia kwa jitihada zake za kuwezesha makundi yote ya Watanzania, wakiwemo vijana.
ISHARA YA MWAMKO MPYA
Uzinduzi wa Serene Safari Bureau de Change unaashiria mwamko mpya wa wanawake na vijana katika kuchangia maendeleo ya taifa kupitia sekta ya kifedha. Ni ishara ya nafasi kubwa ya uwekezaji na mchango wa kizazi kipya cha Watanzania katika kujenga uchumi wa taifa.
Tanzania inaendelea kupiga hatua kubwa katika sekta ya fedha ambapo kijana mwekezaji wa kike, Mishel Mrema, amepongeza jitihada za Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kupigania ndoto za vijana wa Kitanzania na kutoa fursa za kufanya uwekezaji bila ubaguzi.
Alisema anamshukuru Rais Samia kwa kupambania vijana katika kipindi chake cha urais kwa kunyanyua vijana.
Mrema aliongeza kuwa Rais ameweza kuinua vijana kupitia nyanja mbalimbali ikiwemo kilimo, utalii, uchumi na huduma za kifedha kama Bureau de Change. Pia alibainisha kuwa kupitia Royal Tour, wageni kutoka mataifa mbalimbali wamefanikisha fursa nyingi za huduma za kifedha nchini.
Aidha, alitoa wito kwa wananchi pamoja na wageni kutembelea taasisi hiyo ili kubadilishana fedha jijini Arusha, akibainisha kuwa Serene Safari Bureau de Change inalenga kutoa huduma bora za ubadilishaji fedha za kigeni sambamba na kusaidia vijana kupata ajira.
VIONGOZI WAPONGEZA HATUA HIYO
Mgeni rasmi katika hafla ya uzinduzi huo jijini Septemba 27,2025, Iris Naushad Makere, Kamishna wa Mkoa wa Tanzania Girl Guides, alisema kuwa maadili, bidii na roho ya kujituma vimekuwa dira ya maendeleo ya taasisi hiyo. Aliongeza kuwa kuanzishwa kwa taasisi ya kifedha kama Serene Safari Bureau de Change ni ubunifu wenye mchango mkubwa katika kukuza uchumi wa taifa la Tanzania.
Kwa upande wake, Hashim Chamani, Mkurugenzi wa Furaha Safari Bureau de Change, alieleza furaha yake kwa ujio wa taasisi hiyo mpya akisisitiza kuwa itaongeza ushindani wa kibiashara, kuboresha huduma za kifedha na kuchangia ajira kwa vijana. Chamani pia alimpongeza Rais Samia kwa jitihada zake za kuwezesha makundi yote ya Watanzania, wakiwemo vijana.
ISHARA YA MWAMKO MPYA
Uzinduzi wa Serene Safari Bureau de Change unaashiria mwamko mpya wa wanawake na vijana katika kuchangia maendeleo ya taifa kupitia sekta ya kifedha. Ni ishara ya nafasi kubwa ya uwekezaji na mchango wa kizazi kipya cha Watanzania katika kujenga uchumi wa taifa.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...