Na Pamela Mollel, Arusha.

Vijana nchini wametakiwa kuchangamkia fursa ya uwekezaji katika ufugaji wa kuku wa kienyeji, kwa kuwa ni biashara yenye faida kubwa na soko pana linalokua kila siku.

Akizungumza na vijana waliomtembelea katika soko la Morombo jijini Arusha, mjasiriamali maarufu wa kuku, Mudy Musa, alisema ufugaji wa kuku wa kienyeji ni miongoni mwa sekta rahisi kuanza na inaweza kumuwezesha kijana kupata kipato cha haraka endapo atajituma na kuwa na maarifa sahihi.

“Ufugaji wa kuku wa kienyeji unaweza kukupa faida ya haraka kwa sababu nyama na mayai yake hupendwa zaidi na wateja. Ni rahisi kulinganisha na aina nyingine za ufugaji, na soko lake halina kikomo,” alisema Musa.

Aliongeza kuwa mbali na kuuza mayai na nyama, mfugaji anaweza pia kufanya biashara ya kununua kuku kutoka vijijini na kupeleka mjini, jambo linaloweza kumpatia faida kubwa zaidi.

Mudy aliwataka vijana kuiona fursa hii kama njia ya kuondokana na changamoto ya ajira na kujijengea maisha bora kupitia juhudi zao wenyewe.

Vijana waliokutana naye walionesha kufurahishwa na elimu waliyoipata moja kwa moja kutoka kwa mjasiriamali huyo, na walisema wamepata hamasa ya kuanzisha miradi ya ufugaji wa kuku wa kienyeji.

“Tumejifunza mengi. Ufugaji huu siyo tu chanzo cha kipato, bali pia unatoa uhakika wa chakula bora kwa jamii,” alisema mmoja wa vijana hao kwa furaha.




Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...