Wadau mbalimbali wa maendeleo wameendelea kuunga mkono juhudi za serikali hususani katika sekta ya afya ili kuboresha huduma za afya katika maeneo mbali mbali nchini.

Mwenge wa uhuru ukiwa wilayani mbogwe mkoani Geita, umefanikiwa kutembelea na kuweka jiwe la msingi katika kituo binafsi cha afya cha Kagala kilichopo katika halmashauri ya wilaya ya mbogwe.

Kituo cha afya Kagala kimegharimu takribani kiasi cha sh bilioni tatu ambapo kitaenda kupunguza msongamano kwenye vituo vya afya vya maeneo ya karibu.

Kiongozi wa mbio za mwenge 2025 Ismail Ali Ussi amewataka wawekezaji wengine kujitokeza kufanya uwekezaji ili kupanua huduma mbalimbali za kijamii.

Mkurugenzi mtendaji wa kituo cha afya cha Kagala Bunga Dadu amesema kuwa mradi huo umelenga kutoa huduma bora ya afya, kupunguza vifo vya mama na mtoto pamoja na kupunguza adha ya kufata huduma mbali.



Next
This is the most recent post.
Previous
Older Post

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...