Wananchi wanaendelea kuelimishwa  kuhusu ufugaji wa nyuki kuwa ni fursa kubwa ya kipato na maisha bora kwani nyuki wanatupa asali yenye thamani kubwa sokoni, lakini pia wanasaidia kuchavusha mazao yetu na kulinda uhai wa mazingira.

Ni muhimu wadau na wananchi mbalimbali kubadilika na kuacha kutumia moto wakati wa kuvuna asali kwani moto unaharibu mizinga, unaua nyuki na kuunguza misitu yetu, hivyo ukitumia mbinu hizo za kizamani zinapoteza siyo tu nyuki bali pia rasilimali muhimu za misitu na uoto wa asili.

Wananchi wanakumbushwa kuchagua mbinu za kisasa za kuvuna asali ambazo ni mbinu rahisi, salama na zinazohifadhi nyuki pamoja na mazingira yake. 

Aidha inasisitizwa  kuwa kutumia njia hizi zitalinda misitu na kuepelekea kupata asali bora zaidi na kuendelea kutunza misitu kwani utabaki urithi mzuri wa kijani kwa manufaa ya kizazi cha sasa na  vizazi vijavyo.




Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...