Na Mwandishi Wetu

Rais wa Klabu ya Yanga, Mhandisi Hersi Said amesema kuwa walikataa kumuuza Mshambuliaji Clement Mzize kwenye klabu yoyote kutokana na umuhimu na mchango wake kwenye klabu.

Kwenye Mkutano Mkuu wa mwaka wa klabu hiyo uliofanyika Super Dome, Masaki, Dar es Salaam, Mhandisi Hersi amesema kuwa ofa nyingi zilikuja klabuni hapo kumtaka Mzize.

“Ofa ya mwisho iliyokuja kwa Mzize ni USD Milioni mbili (karibu Tsh. Bilioni 5) lakini sisi kwa manufaa ya Klabu yetu tukasema Mzize haendi popote na atabaki hapa Jangwani kuipambania nembo ya klabu,” amesema Eng. Hersi

Vile vile, Hersi amesema kuwa kwa malengo ya klabu hiyo, hawawezi kukuza Wachezaji wenye vipaji na kuwauza kwa wapinzani wengine. Hivyo, wametimiza matakwa yote ya Mchezaji ambayo alihitaji ili kubaki kikosini hapo ili kupambania nembo ya klabu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...