Na Mwandishi  Wetu,Zanzibar 

Chama Cha Mapinduzi (CCM)  kimewatoa hofu  Wazanzibari kuwa  ahadi zote  za kisera  zilizoainishwa katika Ilani  ya Uchaguzi  ya CCM  2025-2030 zitatekelezwa na   Rais wa Zanzibar  Dk Hussein  Ali Mwinyi bila  longolongo. 

Pia chama hicho  kimesisitiza kuwa, kitasimama kama Manyapara  ili kuhakikisha kila  ahadi  inatimizwa kwa wakati .

Hayo yameelezwa leo Novemba 25,2025 na Katibu  wa Kamati  Maalum  ya NEC  Zanzibar, Idara ya Itikadi  ,Uenezi na Mafunzo ,Khamisi  Mbeto Khamis mbele  ya waandishi   wa habari baada ya kumalizika Kikao cha Kamati Maalum ya NEC  Zanzibar. 

Kikao hicho  cha  Kamati Maalum ya NEC  Zanzibar, kimekutana chini  ya Makamo  Mwenyekiti  wake, Rais Dk Mwinyi  katika Afisi  Kuu ya CCM,Kisiwandui mjini Unguja. 

Mbeto  alisema Msimamizi namba moja  wa utekelezaji  wa sera za  chama ,ni chama  chenyewe , ambacho kitafuatilia   kila sekta na kuhakikisha  ahadi zote zimetekelezeka.

Alisema   baada ya wataalam  wa chama kuandika  ilani ,  hatimae ikapitishwa na mkutano  Mkuu wa Taifa wa CCM  ,kazi  ya usimamizi na ufuatiliaji itabaki mikononi mwa   vongozi wa chama  kuanzia  matawi hadi Taifa.

'Napenda niwatoe hofu Wazanzibari  kupitia  kwenu  wana habari.Kazi  ya utekelezaji wa ahadi itafanywa na chama katika ngazi  zake. Kwa utekelezaji wa Sekta za Umma kazi itafanywa na watendaji  wa SMZ 'Alisema  Mbeto 

Aidha, Katibu huyo Mwenezi aliongeza kusema kuwa CCM ndicho kilichoshinda Uchaguzi  Mkuu,kina ridhaa ya wananchi hivyo  kaz iliobaki ni kuhakikisha inasimamia utekelezaji wa sera zake .

"Tutapita  kila kona ya  sekta za umma  kufuatilia  utekelezaji wa ahadi . Tukikuta  mahali mambo  hayaendi tunavyotaka   tutaziarifu Mamlaka husika zichukue hatua stahiki  "Alieleza 

Mwenezi  alisema sababu  ya CCM  kupata  ushindi wa kishindo, imetokana na utelelezaji makini,usio na urasimu  wala ngojangoja katika miaka mitano  iliopita.

"Wananchi wanapoahidiwa ahadi wangependa  kuona matokeo ya ahadi  hizo  zikitekelezwa na serikali  yao si jambo jingine "Alisisitiza Mbeto .

Hata hivyo,Mbeto ametoa wito kwa Wabunge,Wawakilishi na Madiwani wa CCM  kuhakikisha wanatimiza ahadi za kisera na zaki binafsi kwa muda na wakati bila  kutoa visingizio.



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...