JESHI la Polisi Mkoa wa Mbeya linamshikilia Tadesa Limoli [32] raia wa nchini Ethiopia na wenzake 37 wote wanaume kwa kosa la kuingia nchini kinyume cha sheria.

Watuhumiwa walikamatwa mnamo Novemba 11, 2025 huko katika Pori la ranchi ya Matebete lililopo katika Kijiji cha Igumbilo Shamba, Kata ya Chimala, Tarafa ya Ilongo, Wilaya ya Mbarali, Mkoani Mbeya wakisafiri kwa kutumia Gari yenye namba za usajili T.953 DJF aina ya Toyota Noah mali ya Stanslaus Mazengo [51] Mkazi wa Isitu ambaye ndiye alikuwa akiendesha Gari hiyo.

Mtuhumiwa Stanslaus Mazengo ameeleza kuwa alikuwa akiwapeleka kuwahifadhi Wahamiaji hao kwenye nyumba ya Jackline Malya [26] Mkazi wa Chimala. Watuhumiwa walikuwa wakiwasafirisha Wahamiaji hao kwa njia ya kificho kwa lengo la kuwapeleka nchini Afrika ya Kusini.

Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linatoa rai kwa baadhi ya wananchi wenye tamaa ya fedha kuacha tabia ya kuwawezesha raia wa kigeni kuingia ama kupita nchini bila kufuata utaratibu wa kisheria na badala yake wawaelekeze kufuata taratibu kupitia mamlaka husika ili kuepuka usumbufu ikiwemo kukamatwa na kuchukuliwa hatua za kisheria.

Imetolewa na:
Kamanda wa Polisi,
Mkoa wa Mbeya.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...