Arusha

Wanunuzi wa madini kutoka maeneo mbalimbali nchini wameendelea kujitokeza katika Kituo cha Jemolojia Tanzania (TGC) jijini Arusha, wakikagua na kuhakiki ubora wa madini yatakayouzwa katika Mnada wa Tatu wa Madini ya Vito unaotarajiwa kufanyika tarehe 27 Novemba 2025.

Ukaguzi huo ni hatua muhimu inayolenga kuhakikisha uwazi, ushindani na ongezeko la thamani ya madini nchini, kwa kuwa madini yote yatakayopatikana kwenye mnada huo wa kidigitali lazima yakidhi viwango na thamani halisi ya soko.

Mnada huo umeendelea kuvutia wanunuzi wengi wa ndani, jambo linalopanua fursa za kibiashara na kuimarisha mchango wa sekta ya madini katika ukuaji wa uchumi wa taifa.

Aidha, unafungua milango kwa wachimbaji na wauzaji kuongeza wigo wa soko kupitia mfumo wa kisasa na salama wa uuzaji.

Hatua hizi ni sehemu ya jitihada za Serikali kupitia Tume ya Madini kwa kushirikiana na Soko la Bidhaa Tanzania (TMX), kuhakikisha mifumo ya usimamizi na mauzo ya madini inakuwa ya kisasa na yenye tija kwa wananchi na taifa kwa ujumla.







Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...