Baraza la madiwani Halmashauri ya wilaya ya Geita limemchangua diwani wa kata ya Lutede iliyopo mamlaka ya mji mdogo wa Katoro ndugu Jumanne Misungwi kuwa mwenyekiti wa baraza hilo.

Ni katika kikao cha kwanza cha baraza la madiwani wa halmashauri ya wilaya ya Geita ambapo jumla ya madiwani 51 katika wilaya hiyo wameapishwa kuitumikia Halmashauri hiyo.

Mwenyekiti Misungwi amewashukuru madiwani hao kwa kumuamini na kumchagua kuwa kiongozi wa vikao vya madiwani vitakavyokuwa vinafanyika.

Aidha amewaomba ushirikiano ili kuwatumikia wananchi na kuleta maendeleo katika halmashauri hiyo.






Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...