-Washukuru kufikishiwa majiko banifu kwa bei ya ruzuku
Wananchi wa Kijiji cha Mtakuja Kata ya Kapalala katika Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo Mkoani Katavi wameipongeza Serikali kwa kuweka ruzuku kwenye majiko banifu hatua ambayo wamesema inawezesha mwananchi wa kipato chochote kutumia Nishati Safi ya Kupikia
Wametoa pongezi hizo kwa nyakati tofauti Desemba 19, 2025 wakati wa zoezi la usambazaji wa majiko banifu yanayouzwa kwa bei ya ruzuku kijijini hapo unaotekelezwa na Kampuni ya Tango Energy Limited chini ya uratibu na usimamizi wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA).
“Tunaipongeza na kuishukuru Serikali kwa kuweka ruzuku katika bidhaa za nishati safi ya kupikia ikiwemo haya majiko banifu; mpango huu utamfikia kila mwananchi hata yule wa kipato kidogo; Serikali imeamua kutusapoti nasi tumejitoa kama watanzania kuunga jitihada hizi za Serikali,” alisema Felix Milwano Mkazi wa Kijiji cha Kapalala
Kwa upande wake Nelia Fungameza alisema jiko banifu litampunguzia gharama za maisha kwani hapo awali alikuwa akitumia gunia moja la mkaa ndani ya mwezi mmoja lakini kutokana na ufanisi wa majiko hayo kama alivyoelezwa na wataalam ataweza kutumia gunia moja kwa zaidi ya miezi miwili.
Mbali na kupunguza gharama, Fungameza aliishukuru Serikali kwa dhamira yake ya kuboresha afya za wananchi wake kwani kwa kutumia majiko banifu alisema kwa namna alivyoshuhudia likifanya kazi halitoi moshi kama majiko mengine waliokuwa wakitumia hapo kabla.
“Haya majiko banifu mimi sifa zake nilielezwa na rafiki yangu yeye yupo Dar es Salaam, alinieleza ubora na ufanisi wake namna ambavyo yanafanya kazi na namna ambavyo yanaokoa gharama, leo nafarijika yamefika kwetu tena kwa bei ya ruzuku kwa hili naipongeza Serikali,” alisema Maiko Maseki.
Akizungumza wakati wa zoezi la uuzaji wa majiko hayo kwa bei ya ruzuku, Mtaalam wa Nishati na Jinsia kutoka Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Dkt. Joseph Sambali alipongeza mwitikio wa wananchi na aliwasisitiza kuwa mabalozi kwa wananchi wengine ambao hawakupata fursa ya kujipatia majiko hayo.
Alisema kuwa mwitikio huo mkubwa wa wananchi wa kujipatia majiko banifu kwa bei ya ruzuku kunadhihirisha kuwa uelewa kuhusu matumizi ya nishati safi ya kupikia katika kulinda afya na kuhifadhi mazingira umeongezeka miongoni mwa wananchi.
“Zoezi hili la uuzaji wa majiko Mkoani Katavi kwa bei ya ruzuku ya shilingi 7,500 linaendelea, nawasihi wananchi waendelee kujitokeza kwa wingi waendelee kuchangamkia fursa hii kwani bei ya soko kwa jiko moja yaani bila ruzuku jiko hili huuzwa kwa shilingi 59,000,” alifafanua Dkt. Sambali.
Naye Mkurugenzi wa Kampuni ya Tango Energy Ltd, Musa Msofe alitoa wito kwa wananchi wanaofika kujipatia majiko banifu kwa bei ya ruzuku kuhakikisha wanakuwa na vitambulisho vya Taifa (NIDA) ili kuepuka usumbufu na kushindwa kupata huduma.
“Mwananchi anayefika hapa kujipatia jiko ahakikishe anakuja na kadi yake ya NIDA na huu ndio utaratibu nje ya hapo hatoweza kuhudumiwa; tumeanza rasmi uuzaji wa majiko hapa Nsimbo na tutakuwa na tutakuwa na vituo vitano vya uuzaji na tutatangaza ili kila mwananchi aelewe ratiba yetu,” alisema Msofe.
Alisema wamejipanga vyema kuhakikisha zoezi la uuzaji wa majiko hayo linakwenda kama ilivyoelekezwa na Serikali na kwamba kabla ya kuuza wanatoa elimu kuonyesha namna ambavyo majiko hayo yanafanya kazi sambamba na kumuonyesha mwananchi faida za kutumia majiko banifu.
Wananchi wa Kijiji cha Mtakuja Kata ya Kapalala katika Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo Mkoani Katavi wameipongeza Serikali kwa kuweka ruzuku kwenye majiko banifu hatua ambayo wamesema inawezesha mwananchi wa kipato chochote kutumia Nishati Safi ya Kupikia
Wametoa pongezi hizo kwa nyakati tofauti Desemba 19, 2025 wakati wa zoezi la usambazaji wa majiko banifu yanayouzwa kwa bei ya ruzuku kijijini hapo unaotekelezwa na Kampuni ya Tango Energy Limited chini ya uratibu na usimamizi wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA).
“Tunaipongeza na kuishukuru Serikali kwa kuweka ruzuku katika bidhaa za nishati safi ya kupikia ikiwemo haya majiko banifu; mpango huu utamfikia kila mwananchi hata yule wa kipato kidogo; Serikali imeamua kutusapoti nasi tumejitoa kama watanzania kuunga jitihada hizi za Serikali,” alisema Felix Milwano Mkazi wa Kijiji cha Kapalala
Kwa upande wake Nelia Fungameza alisema jiko banifu litampunguzia gharama za maisha kwani hapo awali alikuwa akitumia gunia moja la mkaa ndani ya mwezi mmoja lakini kutokana na ufanisi wa majiko hayo kama alivyoelezwa na wataalam ataweza kutumia gunia moja kwa zaidi ya miezi miwili.
Mbali na kupunguza gharama, Fungameza aliishukuru Serikali kwa dhamira yake ya kuboresha afya za wananchi wake kwani kwa kutumia majiko banifu alisema kwa namna alivyoshuhudia likifanya kazi halitoi moshi kama majiko mengine waliokuwa wakitumia hapo kabla.
“Haya majiko banifu mimi sifa zake nilielezwa na rafiki yangu yeye yupo Dar es Salaam, alinieleza ubora na ufanisi wake namna ambavyo yanafanya kazi na namna ambavyo yanaokoa gharama, leo nafarijika yamefika kwetu tena kwa bei ya ruzuku kwa hili naipongeza Serikali,” alisema Maiko Maseki.
Akizungumza wakati wa zoezi la uuzaji wa majiko hayo kwa bei ya ruzuku, Mtaalam wa Nishati na Jinsia kutoka Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Dkt. Joseph Sambali alipongeza mwitikio wa wananchi na aliwasisitiza kuwa mabalozi kwa wananchi wengine ambao hawakupata fursa ya kujipatia majiko hayo.
Alisema kuwa mwitikio huo mkubwa wa wananchi wa kujipatia majiko banifu kwa bei ya ruzuku kunadhihirisha kuwa uelewa kuhusu matumizi ya nishati safi ya kupikia katika kulinda afya na kuhifadhi mazingira umeongezeka miongoni mwa wananchi.
“Zoezi hili la uuzaji wa majiko Mkoani Katavi kwa bei ya ruzuku ya shilingi 7,500 linaendelea, nawasihi wananchi waendelee kujitokeza kwa wingi waendelee kuchangamkia fursa hii kwani bei ya soko kwa jiko moja yaani bila ruzuku jiko hili huuzwa kwa shilingi 59,000,” alifafanua Dkt. Sambali.
Naye Mkurugenzi wa Kampuni ya Tango Energy Ltd, Musa Msofe alitoa wito kwa wananchi wanaofika kujipatia majiko banifu kwa bei ya ruzuku kuhakikisha wanakuwa na vitambulisho vya Taifa (NIDA) ili kuepuka usumbufu na kushindwa kupata huduma.
“Mwananchi anayefika hapa kujipatia jiko ahakikishe anakuja na kadi yake ya NIDA na huu ndio utaratibu nje ya hapo hatoweza kuhudumiwa; tumeanza rasmi uuzaji wa majiko hapa Nsimbo na tutakuwa na tutakuwa na vituo vitano vya uuzaji na tutatangaza ili kila mwananchi aelewe ratiba yetu,” alisema Msofe.
Alisema wamejipanga vyema kuhakikisha zoezi la uuzaji wa majiko hayo linakwenda kama ilivyoelekezwa na Serikali na kwamba kabla ya kuuza wanatoa elimu kuonyesha namna ambavyo majiko hayo yanafanya kazi sambamba na kumuonyesha mwananchi faida za kutumia majiko banifu.












Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...