MKUU wa mkoa wa Kilimanjaro, Nurdin Babu akisaini kitabu cha maombolezo kufuatia kifo cha aliyekuwa Mkuu wa mkoa wa Njombe na Mara mwaka 2012/2016, Kapteni Aseri Msangi nyumbani kwa marehemu Chekereni wilayani Moshi.
Kapteni Msangi aliyehudumu katika nafasi mbalimbali za uongozi ndani ya Serikali na Chama cha Mapinduzi ikiwemo ukuu wa wilaya za Geita, Mwanza, Musoma, Ngorongoro, Nanyumbu na Iringa akifariki Dunia Januari 2 mwaka huu katika hospitali ya rufaa ya kanda ya Kaskazini KCMC.
Kwa mujibu wa familia, marehemu atazikwa kesho nyumbani kwake Chekereni wilayani Moshi.




Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...