WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba amewaagiza watendaji wa Serikali kuandaa jedwali la kuonesha namna walivyotatua kero za wananchi katika kila wiki ya mwisho wa mwezi.

Amesema hayo leo Jumapili (Machi 01, 2026) katika mkutano wa hadhara uliofanyika Stendi za Zamani, Babati Mjini mkoani Manyara.

Amesema kuwa Serikali haiwezi kukubali utaratibu wa kulimbikiza matatizo ya watu kana kwamba Serikali haipo.

Ameongeza kuwa Serikali imetengeneza utaratibu ndani ya nchi wa kuwa na uongozi katika kila eneo kwa ajili ya kuwarahisishia wananchi kupata ufumbuzi wa matatizo yao.

“Hatukutengeneza ofisi hizi za Serikali ili kugawana vyeo. Ninawahakikishia tukianza kufuatilia tutajua nani anaweza kazi na anastahili kukaa ofisini.”





Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...