Kibaha, Pwani
CCM leo imekuwa mwenyeji wa mkutano kati ya Chama cha Kikomunisti cha China (CPC) na Vyama Sita Rafiki vya Ukombozi Kusini mwa Afrika uliofanyika katika Shule ya Uongozi ya Mwalimu Julius Nyerere (MJNLS), Kibaha.
Mkutano huo chini ya wenyeji wa Chama Cha Mapinduzi, ulikuwa sehemu ya ziara ya kikazi ya Komredi Liu Haixing, Mjumbe wa Kamati Kuu na Waziri wa Idara ya Mambo ya Nje wa CPC kutoka China.
Katika mkutano huo, viongozi wa vyama vya ukombozi kutoka ANC, FRELIMO, MPLA, SWAPO na ZANU-PF walijadiliana na CPC kuhusu kuimarisha mshikamano, kubadilishana uzoefu wa kiuongozi na kusukuma ajenda ya maendeleo ya kisasa kwa ustawi wa wananchi wao.
Viongozi hao pia walishiriki uzinduzi wa Kituo cha Tafiti kuhusu Fikra za Xi Jinping juu ya Ujamaa wenye Maono ya Kichina katika Zama Mpya, hatua inayolenga kuimarisha ushirikiano wa kielimu na maendeleo kati ya CCM na CPC.
.jpeg)



.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...