Mwanandishi wetu, Morogoro.
WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais, Mhe. Mhandisi Hamad Masauni amesema Usimamizi na uhifadhi wa mazingira hauwezi kufanikiwa kwa kauli au sera peke yake, bali kwa vitendo vinavyoonekana katika ngazi zote ikiwemo shughuli za kupanda miti na kuitunza.
Amesema maono na Matarajio ya Dira 2050 ni makubwa na yanahitaji ubunifu mkubwa katika kufanya kazi ili kufikia matarajio hasa katika mikakati mahsusi ya hifadhi na ustahimilivu wa mabadiliko ya tabianchi.
Waziri Masauni ameyasema hayo Mei 15, 2026 wilayani Kilosa mkoani Morogoro kwenye zoezi la upandaji miti ili kuhakikisha mazingira yanabaki kuwa salama kutokana na uoto wa asili ikiwa moja shughuli zilizopangwa na Ofisi ya Makamu wa Rais kuelekea Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani itakayofanyika Juni 5 mwaka huu ambapo kitaifa itafanyika mkoani Dodoma.
Amesema Dira ya Taifa ya mwaka 2050 ina nguzo kuu tatu na miongoni mwa nguzo hizo ni suala zima la uhifadhi wa mazingira na utahimilivu wa mabadiliko ya tabianchi jambo ambalo kila mmoja anapaswa kulitazama kwa upana wake.
"Haya tunayoyaona hapa kama vile athari za mafuriko, hali ya hewa isiyotabilika inayosababisha ukame na madhara mengine mengi miongoni mwa sababu zake ni mabadiliko ya tabianchi, hivyo kama taifa ni lazima tutoe kipaumbele katika kuhakikisha athari za mabadiliko ya tabianchi tunazihimili," amesema Masuni.
Ameongeza kuwa mtu anaweza asione faida ya upandaji miti lakini ukweli ni kuwa miti hiyo inafaida kuwa katika suala zima la upandaji miti hasa kwa kizazi kichacho cha miaka 50 ijayo kwani ndiyo wenye Tanzania ya baadaye.
Aidha Waziri Masauni aliipongeza Wilaya ya Kilosa na mkoa mzima wa Morogoro kwa kuwahusisha wananafuzi wa shule za msingi na sekondari katika suala zima la upandaji miti na utunzaji mazingira.
Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Kilosa, Mhe. Shaka Hamdu Shaka kwa niaba ya Mkuu wa mkoa wa Morogoro alisema kuwa wilaya hiyo imejiwekea malengo ya kupanda miti milioni 1.5 na kwamba zoezi hilo limekuwa likifanyika kila mwaka kwa mfululizo wa miaka mitano.
Mhe. Shaka amesema kuwa wilaya yake mara kwa mara imekuwa ikikubwa na mafuriko na kwamba katika kukabiliana na hali hiyo, serikali imedhamilia kujenga mabawa ya maji katika maeneo ya mto Mkondoa ili kuweza kudhibiti mafuriko, hivyo zoezi la upandi miti hiyo kutasaidia kulinda na kufidhi bwawa hilo na hivyo kuchochea maendeleo mbalimbali ya kiuchumi..jpg)
.jpg)


.jpg)
.jpg)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...