Na  MWANDISHI WETU

DIWANI wa Kata ya kisutu, jijini Dar es Salaam, kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi CCM)  , Tousif Bhojani, ameibua shangwe kwa wakazi wa eneo hilo baada ya kuzipatia ufumbuzi kero mbalimbali  zilizo kuwa zikiwakabili.

Bhojani  ametatua karo mbalimbali  za wananchi katika mkutano wa hadhara  wa kusikiliza na kutatua kero  uliofanyika katika Viwanja vya Soko la Kisutu, ambao ulihusisha pia  wataalamu kutoka taasisi mbalimbali za serikali ambao walizitolea majibu baadhi ya  changamoto.

Kero hizo ni pamoja na ukosefu wa kisima cha maji katika Soko la Baba na Mamalishe Kisutu, kuvuja kwa paa la soko hilo na ukosefu wa vifaa vya zimamoto.

Changamoto zingine ni maegesho, kero ya kamata kamata ya  'wrong parking', ulinzi na usalama, mikopo ya asilimia 10 inayotolewa na halmashauri na  utirikaji wa maji taka.

Katika kutatua  changamoto ya Soko la Mama na Baba Lishe Kisutu kutokuwa na kisima, Diwani Bhojani aliwasiliana kwa simu papo hapo   na Spika wa Bunge  ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Ilala, Mussa Hassan Zungu, ambaye  aliwahutubia wananchi kwa njia ya simu na kuahidi kushirikiana na diwani huyo kutatua kero hiyo.

Akizungumza kwa njia ya simu Spika Zungu amewataka wananchi kushikamana, kuwa wamoja na kuahidi kero mbalimbali  kuwa zitatuliwa kwa kushirikiana na diwani wao huyo, jambo lililozua shangwe.

"Baada ya kukata simu Spika na Mbunge wetu Zungu, amenitumia ujumbe kuwa tutahakikisha kisima cha maji kina jengwa hapa.Kuhusu paa  la soko kuvuja  nimewasiliana hapa hapa na Mkurugenzi wa Jiji la Dar es Salaam, Elihuruma Mabelya, ameahidi kuja mwenyewe  kukagua na kuna kushughulikia kero hiyo,"amesema Diwani Bhojani.

Diwani huyo pia ameahidi kutoa kifaa cha kuzimia moto katika soko hilo mapema wiki ijayo.

Kuhusu changamoto ya ubovu wa barabara kutokana mvua iliyonyesha, Diwani Bhojani ameahidi kuiwasilisha kwa Wakala wa Barabara Mjini na Vijijini (TARURA) ili kurekebishwa.

Akizungumzia ulinzi na usalama, diwani huyo amesema kuna vikundoi vya sungusungu v kwa kushirikiana na Jeshi la polisi, vinaimarisha ulinzi katika kata hiyo hivyo kuwatoa hofu na kuwataka kuchangia  ada ya ulinzi. 

Changamoto zingine zilijibiwa na  taasisi za serikali hususan  Jeshi la Zimamoto na Ukoaji, ambalo liliahidi kufanya ukaguzi katika soko hilo.

Kwa upande wa kero  ya maji  Mwakilishi wa Mamlaka ya Majisafi na  Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA) amewatoa wasaiwasi wananchi kuhusu upatikanaji wa maji kwamba mamlaka hiyo  inaendelea kuimarisha mifumo yake kuhakikisha maji yanapatikana wakati wote.

Kuhusu mikopo ya asilimia 10 inayotolewa na Halmashauri ya Jiji la Dar es  Salaam,  mwakilishi kutoka jiji hilo, amesema kata hiyo imenufaika na mikopo  ya jumla ya sh. milioni 169 ambazo zimetolewa kwa vikundi vitano, hivyo kuwataka wananchi kuunda vikundi  kwani mikopo hiyo ipo na inaendelea kutolewa.

Wananchi wa kata hiyo wamempongeza Diwani Bhojani kwa utaratibu wa kuandaa mikutano na kusikiliza kero zao  kwani ni njia rahisi ya kutatua kero hizo kabla hazijaleta adha kubwa.









 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...