IDARA ya Utalii kwa kushirikiana na Kitengo cha Mawasiliano cha Wizara ya Maliasili na Utalii imesema inatarajia kuanza mchakato wa kupanga hadhi (Grading and regrading) kwa watoa huduma wa hoteli na chakula nchini.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo Ijumaa Mei Mosi, 2026, na Mkurugenzi wa Idara ya Utalii Dkt. Thereza Mugobi, mchakato huo ambao ni wa kawaida ni hatua muhimu ya kujiandaa na ongezeko kubwa la wageni linalotarajiwa kuingia na kuhudumiwa nchini wakati wa michuano ya kuwania Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON-2027)
Pia amesema unalenga kuinua ubora wa huduma ili kuiwezesha Tanzania kujitangaza kimataifa kama kitovu cha utalii na ukarimu barani Afrika huku akidokeza kuwa zoezi hilo litaanza mwanzoni mwa mwezi Mei hadi Juni 2026 katika mikoa ya Dar es Salaam, Morogoro na Kilimanjaro.
Zoezi hilo litahusisha ukaguzi wa kina wa miundombinu, usafi, ubora wa chakula, pamoja na huduma kwa wateja ili kuhakikisha zinakidhi viwango vya kimataifa.
Amewataka wamiliki na watoa huduma wa hoteli kutumia fursa hiyo kujipima kiwango cha ubora wa huduma huduma wanazotoa ili kuvutia na kuwahifadhi wageni kabla, wakati na baada ya AFCON-2027.
Kupitia zoezi hilo, hilo hadhi ya nyota kwa hoteli itatolewa huku likizingatia ubora wa hadhi ya nyota 5 ambapo zilizokidhi zitapandishwa hadhi na zile zisizokidhi zitashushwa hadi hiyo.



Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...