Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi amemwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika Mazishi ya aliyekuwa Askofu wa Pili wa Kanisa la Anglikana Dayosisi ya Ruvuma na Katibu Mkuu Mstaafu wa Jumuiya ya Kikristo Tanzania (CCT) Marehemu Askofu Stanford Shauri.

Mazishi hayo yamefanyika katika Kanisa la Anglikana Dayosisi ya Ruvuma, Liuli Wilaya ya Nyasa mkoani Ruvuma.

Akitoa salamu za rambirambi kwa niaba ya Rais. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Makamu wa Rais amesema Serikali inatambua mchango mkubwa aliyoutoa Askofu Shauri katika hapa nchini, akiwa ametumikia Serikali za Mitaa kwa zaidi ya miaka 12 pamoja na kuwa katibu mkuu wa Jumuiya ya Kikristo Tanzania (CCT) kwa zaidi ya miaka 10.

Aidha, Makamu wa Rais amesema Marehemu Askofu Shauri amekuwa na mchango mkubwa katika maendeleo ya jamii pamoja na kuendeleza na kuikuza imani ya kikristo nchini.

Amesema ni dhamira ya Serikali kuendeleza yale ambayo Marehemu Askofu Shauri aliyasimamia ikiwemo masuala ya amani na haki.

Makamu wa Rais amewasilisha salamu za pole kwa familia ya marehemu, Kanisa la Anglikana, wakazi wa Ruvuma, Nyasa na wote walioguswa na msiba huo.

Kwa upande wake Askofu Mkuu wa Kanisa la Anglikana Tanzania Maimbo Mndolwa, ameishukuru Serikali kwa ushirikiano mzuri iliyonayo na Taasisi za Dini katika kutoa huduma mbalimbali kwa wananchi. Ameipongeza Serikali kwa ukarabati wa barabara kutoka Mbambabay hadi Liuli katika Wilaya ya Nyasa ambayo ilikuwa ni changamoto kubwa hali inayodhihirisha kuwajali wananchi wa eneo hilo.









Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...