Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Alhaj Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amejumuika na waumini wa dini ya Kiislamu katika dua maalum ya kumuombea marehemu Sheikh Abuubakar bin Said Al-Abassy.
Dua hiyo imesomwa leo, tarehe 02 Mei 2026, katika Ukumbi wa Majid uliopo Kiembe Samaki, Mkoa wa Mjini Magharibi.
Rais Dkt. Mwinyi amemuelezea mwanazuoni huyo kuwa alikuwa mtu mwema, mwenye upendo, na aliyewafundisha watu wengi elimu ya dini.
Wakati huohuo, Rais Dkt. Mwinyi ametoa mkono wa pole kwa Waziri wa Maji, Nishati na Madini, Mhe. Nadir Abdullatif Al-Wardi, pamoja na familia yake kufuatia kifo cha baba yao mzazi aliyefariki nchini India.
Rais Dkt. Mwinyi alifika nyumbani kwa familia hiyo, Chukwani Buyu, kutoa mkono wa pole na kuwataka kuwa na subira katika kipindi hiki cha msiba mzito.
Dua hiyo imesomwa leo, tarehe 02 Mei 2026, katika Ukumbi wa Majid uliopo Kiembe Samaki, Mkoa wa Mjini Magharibi.
Rais Dkt. Mwinyi amemuelezea mwanazuoni huyo kuwa alikuwa mtu mwema, mwenye upendo, na aliyewafundisha watu wengi elimu ya dini.
Wakati huohuo, Rais Dkt. Mwinyi ametoa mkono wa pole kwa Waziri wa Maji, Nishati na Madini, Mhe. Nadir Abdullatif Al-Wardi, pamoja na familia yake kufuatia kifo cha baba yao mzazi aliyefariki nchini India.
Rais Dkt. Mwinyi alifika nyumbani kwa familia hiyo, Chukwani Buyu, kutoa mkono wa pole na kuwataka kuwa na subira katika kipindi hiki cha msiba mzito.


.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)

.jpeg)

Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...