NA Janeth Raphael MichuziTv -Dodoma 

Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa nchini (TAKUKURU) imewafikisha Mahakamani  waliokuwa viongozi wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT) na watendaji wa Wakala wa Ufundi na Umeme Tanzania (TEMESA), wakikabiliwa na mashtaka ya kuunda genge la uhalifu, uhujumu uchumi na utakatishaji fedha kwa kujipatia zaidi ya Sh3.5 bilioni kwa njia za udanganyifu.

Hayo yamesemwa  na Wakili wa serikali mwandamizi Godviver Killian leo  tarehe 25 may 2026  baada ya watuhumiwa hao kufikishwa mahakamani na  kusomewa mashtaka yao katika Mahakama ya hakimu mkazi Jijini Dodoma  TEMESA wakikabiliwa na mashtaka 9 huku CWT  Mastaka 14.

Dodoma: Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa nchini (TAKUKURU) imewafikisha katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Dodoma waliokuwa viongozi wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT) pamoja na watendaji wa Wakala wa Ufundi na Umeme Tanzania (TEMESA), wakituhumiwa kwa makosa ya kuunda genge la uhalifu,  uhujumu uchumi, utakatishaji fedha kwa kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu kiasi cha Sh3.5 bilioni

Kwa upande wa CWT, waliofikishwa mahakamani ni aliyekuwa Rais wa chama hicho Leah Ulaya, Makamu wa Rais Suleimani Ikomba, aliyekuwa Katibu Mkuu Maganga Japhet, pamoja na Joseph Misalaba, Nashon Kidudu, Baraka Mbonalibha, Wambura Kihengu, Angelina Wambura na Kampuni ya Pyrate and Industries Company Limited.

Washtakiwa hao wanakabiliwa na jumla ya mashtaka 14 ya uhujumu uchumi, ikiwemo kujipatia zaidi ya Sh2.2 bilioni kinyume cha sheria kati ya mwaka 2023 na 2024.

Akisoma mashtaka mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Dodoma, Zabibu Mpangule, Mwendesha Mashtaka Mwandamizi wa Serikali, Patrick Mwita amesema washtakiwa hao waliidhinisha matumizi ya fedha hizo kwa ajili ya ununuzi wa tisheti na kofia kinyume na Katiba ya CWT.

Mwita amedai kuwa washtakiwa hao pia walijipatia Sh1.3 bilioni kutoka Kampuni ya Pyrate and Industries Company Limited ili kupitisha zabuni ya ununuzi wa tisheti na kofia hizo kinyume cha taratibu za chama.

Aidha, amewataja wakurugenzi wa kampuni hiyo, Wambura Kihengu na Angelina Wambura, kuwa wanakabiliwa na shtaka la kughushi nyaraka mbalimbali ili kuonyesha kampuni hiyo ilikuwa halali, huku wakifahamu kuwa kitendo hicho ni kosa kisheria.

"Watuhumiwa wengine watatu ambao ni Selemani Ikomba, Baraka Mbonalibha na Angelina Wambura bado wanaendelea kutafutwa ili waunganishwe na wenzao kwenye kesi hii,” alisema Mwita.

Kwa upande wa TEMESA, waliofikishwa mahakamani ni Lazaro Kilahala, Mathias Rutaguza, Sambayeti Magoko, Kennedy Manene, Peter Bongole, Clavery Busunzu, Mbisho Kibuti, Renatha Juma, Vincent Lutembuka, Michael Assey, Caesar Chambo, Nassor Igangule, Deus Matiku pamoja na Kampuni ya Kentra Tanzania Limited.

Washtakiwa hao wanashtakiwa kwa makosa tisa ikiwemo kughushi nyaraka za ununuzi wa vipuri vya magari na kuisababishia Serikali hasara ya zaidi ya Sh1.3 bilioni.

Mwita amesema watuhumiwa wawili, Mathias Rutaguza na Michael Assey, bado wanatafutwa ili waunganishwe katika kesi hiyo.

Kwa upande wake, Hakimu Mkazi Mkuu Zabibu Mpangule amewaeleza washtakiwa kuwa mahakama hiyo haina mamlaka ya kusikiliza kesi za uhujumu uchumi na utakatishaji fedha hadi ipokee kibali maalum kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka kutoka ofisi ya Mwanasheria mkuu wa serikali (DPP).






Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...