Na Janeth Raphael | Michuzi TV

Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) limetoa nafasi ya mwisho kwa vijana waliohitimu elimu ya sekondari ngazi ya Kidato cha Sita mwaka 2026 na kuchaguliwa kujiunga na mafunzo ya JKT kwa mujibu wa sheria, lakini bado hawajaripoti katika makambi waliyopangiwa.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo Juni 12, 2026, jijini Dodoma na Makao Makuu ya JKT, vijana hao wametakiwa kuripoti kuanzia leo hadi Juni 15, 2026 ili kuendelea na mafunzo yao.

Taarifa hiyo imetolewa na Mkuu wa Tawi la Operesheni na Mafunzo JKT, Peter Mnyani, kwa niaba ya Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa, Rajabu Nduku Mabele.

JKT imeeleza kuwa vijana ambao hawakufanikiwa kufika katika makambi waliyoelekezwa awali wanapaswa kuripoti katika kambi za JKT zilizo karibu na maeneo wanayoishi ili kurahisisha usajili na kuendelea na mafunzo.

Hata hivyo, Jeshi hilo limefafanua kuwa utaratibu huo hauhusishi vijana wanaotakiwa kuripoti katika Kambi ya Makutupora JKT Camp, Kambi ya Ruvu JKT Camp pamoja na Kambi ya Chuo cha Uongozi Kimbiji, ambazo hazijajumuishwa katika mwongozo huo wa kuripoti kwenye kambi zilizo karibu.

JKT imewasisitiza vijana wote husika kutumia fursa hiyo ya nyongeza ya muda kuhakikisha wanaripoti ndani ya kipindi kilichotolewa ili kutimiza wajibu wao wa kujiunga na mafunzo kwa mujibu wa sheria na taratibu zilizowekwa.






Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...