Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar itaendelea kuiimarisha mifumo ya usimamizi wa nyaraka za kieletroniki ili kuhakikisha taarifa muhimu za Taifa zinahifadhiwa kwa usalama, zinapatikana kwa urahisi na zinadumu kwa muda mrefu.
Hayo yamemwa na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abulla katika maadhimisho ya siku ya nyaraka duniani kwa mwaka 2026 yaliyoadhimisha kitaifa katika viwanja vya Makumbusho ya Amani Mnazi mmoja.
Amesema katika kipindi hiki cha maendeleo makubwa ya teknolojia ya habari na mawasiliano usimamizi wa nyaraka unahitaji kwenda sambamba na matumizi ya mifumo ya kisasa ya kidijitali ili kurahisha upatikanaji wa taarifa na kuongeza ufanisi zaidi.
Mhe Hemed amesema kuwa ni matumaini ya Serikali kuwa taasisi zote za umma na binafsi zitaendelea kuzingatia viwango vya kitaalamu katika usimamizi wa nyaraka na kumbukumbu kwa lengo la kuongeza ufanisi wa utoaji huduma kwa wananchi na kulinda historia ya Taifa la Tanzania.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar amesema kuwa Zanzibar imekuwa kitovu muhimu cha elimu, biashara, ustaarabu na utamaduni katika ukanda wa Afrika Mashariki na bahari ya hindi hivyo Serikali itahakikisha kuwa Manuskripti zinaendelea kuhifadhi maarifa muhimu yanayohusu dini, sheria, elimu, tiba , biashara, utawala na maisha ya jamii kwa ujumla.
Aidha amesema kuwa hati za kale ni ushahidi tosha wa mchango mkubwa wa Zanzibar katika maendeleo ya elimu na ustaarabu wa kiislamu sambamba na kuwa chanzo muhimu cha tafiti kwa watafiti , wanahistoria, wanafunzi na taasisi mbali mbali duniani.
Sambamba na hilo Mhe. Hemed amesema ni wajibu wa kila mmoja kuhakikisha kuwa manuskripti na nyaraka adhimu zinalindwa, zinatunzwa na zinaendelezwa kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho na kuahidi kuwa Serikali itaendelea kushirikiana na taasisi mbali mbali za ndani na nje ya nchi katika kuhifadhi na kuendeleza urithi huu muhimu kwa Taifa.
Hata hivyo Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar ametoa wito kwa wananchi kuthamini utamaduni wa kutunza kumbukumbu na nyaraka muhimu katika maisha yao binafsi, taasisi na jamii kwa ujumla kwani Taifa lenye utamaduni wa kuhifadhi kumbukumbu zake hujenga msingi imara wa maendeleo, uwajibikaji na utambulisho wa vizazi vyake.
Nae waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Ikulu Mhe. Dkt. SAADA MKUYA SALUM amesema uwepo wa taasisi ya Nyaraka huisaidia jamii kujua umuhimu wa nyaraka na kumbukumbu katika kuhifadhi historia, kulinda haki za wananchi, kuimarisha uwazi na uwajibikaji pamoja na kuchangia maendeleo endelevu katika jamii.
Amesema nyaraka ni msingi wa kumbukumbu za Taifa zinazohifadhi ushahidi wa shughuli za Serikali na jamii pamoja na kulinda haki za wananchi, kuimarisha utawala bora na kutoa rejea muhimu kwa vizazi vya sasa na vijavyo.
Aidha Dkt. Saada amefahamisha kuwa katika kuadhimisha siku ya nyaraka duniani taasisi ya nyaraka na kumbukumbu Zanzibar imeandaa na kutekeleza shughili mbali mbali ikiwewmo jukwaa la nyaraka, ziara za kijamii, maonesho ya nyaraka za kihistoria sambamba na maonesho maalumu ya maandiko ya kiislamu na hati za kiarabu.
Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Nyaraka na kumbukumbu Zanzibar ndugu Khatibu Suleiman Khatibu amesema taasisi hio imejipanga kutoa elimu juu ya matumizi mazuri ya nyaraka na kumbukumbu kwa maslahi ya vizazi vya sasa na baadae.
Ndugu Khatibu ametumia nafasi hio kuitaka jamii kuitumia taasisi ya nyaraka katika utunzaji wa nyaraka na kumbukumbu pamoja na kupata elimu juu ya utunzaji wa nyaraka na kujiepusha na migogoro isiokuwa na tija katika jamii
Mapema Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar amekagua mabanda ya maonesho ya vitu vya asili na tamaduni za kizanzibari.
Hayo yamemwa na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abulla katika maadhimisho ya siku ya nyaraka duniani kwa mwaka 2026 yaliyoadhimisha kitaifa katika viwanja vya Makumbusho ya Amani Mnazi mmoja.
Amesema katika kipindi hiki cha maendeleo makubwa ya teknolojia ya habari na mawasiliano usimamizi wa nyaraka unahitaji kwenda sambamba na matumizi ya mifumo ya kisasa ya kidijitali ili kurahisha upatikanaji wa taarifa na kuongeza ufanisi zaidi.
Mhe Hemed amesema kuwa ni matumaini ya Serikali kuwa taasisi zote za umma na binafsi zitaendelea kuzingatia viwango vya kitaalamu katika usimamizi wa nyaraka na kumbukumbu kwa lengo la kuongeza ufanisi wa utoaji huduma kwa wananchi na kulinda historia ya Taifa la Tanzania.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar amesema kuwa Zanzibar imekuwa kitovu muhimu cha elimu, biashara, ustaarabu na utamaduni katika ukanda wa Afrika Mashariki na bahari ya hindi hivyo Serikali itahakikisha kuwa Manuskripti zinaendelea kuhifadhi maarifa muhimu yanayohusu dini, sheria, elimu, tiba , biashara, utawala na maisha ya jamii kwa ujumla.
Aidha amesema kuwa hati za kale ni ushahidi tosha wa mchango mkubwa wa Zanzibar katika maendeleo ya elimu na ustaarabu wa kiislamu sambamba na kuwa chanzo muhimu cha tafiti kwa watafiti , wanahistoria, wanafunzi na taasisi mbali mbali duniani.
Sambamba na hilo Mhe. Hemed amesema ni wajibu wa kila mmoja kuhakikisha kuwa manuskripti na nyaraka adhimu zinalindwa, zinatunzwa na zinaendelezwa kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho na kuahidi kuwa Serikali itaendelea kushirikiana na taasisi mbali mbali za ndani na nje ya nchi katika kuhifadhi na kuendeleza urithi huu muhimu kwa Taifa.
Hata hivyo Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar ametoa wito kwa wananchi kuthamini utamaduni wa kutunza kumbukumbu na nyaraka muhimu katika maisha yao binafsi, taasisi na jamii kwa ujumla kwani Taifa lenye utamaduni wa kuhifadhi kumbukumbu zake hujenga msingi imara wa maendeleo, uwajibikaji na utambulisho wa vizazi vyake.
Nae waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Ikulu Mhe. Dkt. SAADA MKUYA SALUM amesema uwepo wa taasisi ya Nyaraka huisaidia jamii kujua umuhimu wa nyaraka na kumbukumbu katika kuhifadhi historia, kulinda haki za wananchi, kuimarisha uwazi na uwajibikaji pamoja na kuchangia maendeleo endelevu katika jamii.
Amesema nyaraka ni msingi wa kumbukumbu za Taifa zinazohifadhi ushahidi wa shughuli za Serikali na jamii pamoja na kulinda haki za wananchi, kuimarisha utawala bora na kutoa rejea muhimu kwa vizazi vya sasa na vijavyo.
Aidha Dkt. Saada amefahamisha kuwa katika kuadhimisha siku ya nyaraka duniani taasisi ya nyaraka na kumbukumbu Zanzibar imeandaa na kutekeleza shughili mbali mbali ikiwewmo jukwaa la nyaraka, ziara za kijamii, maonesho ya nyaraka za kihistoria sambamba na maonesho maalumu ya maandiko ya kiislamu na hati za kiarabu.
Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Nyaraka na kumbukumbu Zanzibar ndugu Khatibu Suleiman Khatibu amesema taasisi hio imejipanga kutoa elimu juu ya matumizi mazuri ya nyaraka na kumbukumbu kwa maslahi ya vizazi vya sasa na baadae.
Ndugu Khatibu ametumia nafasi hio kuitaka jamii kuitumia taasisi ya nyaraka katika utunzaji wa nyaraka na kumbukumbu pamoja na kupata elimu juu ya utunzaji wa nyaraka na kujiepusha na migogoro isiokuwa na tija katika jamii
Mapema Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar amekagua mabanda ya maonesho ya vitu vya asili na tamaduni za kizanzibari.










Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...