Na Chalila Kibuda, Michuzi TV
Chama cha Wafanyakazi wa Ukusanyaji wa Mapato Tanzania (TAREWU) kimesaini hati ya makubaliano ya ushirikiano wa miaka mitano na kampuni ya BodyMind Insight (BMI) kwa lengo la kuimarisha afya ya akili, ustawi wa kisaikolojia na maendeleo ya wafanyakazi nchini.
Hafla ya utiaji saini wa makubaliano hayo imefanyika katika ofisi za BMI jijini Dar es Salaam, ambapo viongozi wa pande zote mbili walisisitiza umuhimu wa kuweka afya ya akili katika nafasi ya juu ndani ya mazingira ya kazi.
Akizungumza mara baada ya kusaini makubaliano hayo, Katibu Mkuu wa TAREWU, Dkt. Michael Marere, alisema chama hicho kimeamua kuweka kipaumbele katika kulinda afya ya akili na ustawi wa wanachama wake ili kuongeza ufanisi kazini na kuboresha maisha yao kwa ujumla.
Alisema kupitia ushirikiano huo, wanachama wa TAREWU watapata elimu kuhusu afya ya akili, ustawi wa kisaikolojia na mbinu za kukabiliana na changamoto mbalimbali zinazoweza kuathiri utendaji wao wa kazi.
“Makubaliano haya yatadumu kwa kipindi cha miaka mitano na yanaweza kuongezwa baada ya muda huo kuisha kulingana na mafanikio yatakayopatikana,” alisema Dkt. Marere.
Aliongeza kuwa afya ya akili imekuwa suala muhimu katika mazingira ya kazi ya kisasa na inahitaji kupewa uzito sawa na afya ya mwili kutokana na mchango wake katika kuongeza tija na ubunifu kazini.
“Wafanyakazi wenye afya bora ya akili huongeza ufanisi katika utekelezaji wa majukumu yao na kuchangia maendeleo ya taasisi pamoja na taifa kwa ujumla. Katika mazingira ya kazi yanayobadilika kwa kasi, ni muhimu kuwawezesha wafanyakazi kujenga ustahimilivu wa kukabiliana na changamoto za maisha na kazi,” alisema.
Kwa upande wake, Mkurugenzi wa BMI, John Ambrose, alisema afya ya akili ndiyo msingi wa mafanikio ya mtu binafsi na taasisi, akisisitiza umuhimu wa kujenga mazingira salama yanayozingatia ustawi wa wafanyakazi.
Ambrose alisema changamoto za afya ya akili zinaendelea kuongezeka duniani, huku ripoti ya Afya ya Akili Mahali pa Kazi ya mwaka 2026 ikionyesha kuwa asilimia 61 ya wafanyakazi wameongeza matumizi ya likizo zinazohusiana na afya ya akili mwaka huu.
Aliongeza kuwa asilimia 36 ya wafanyakazi duniani wanakabiliwa na matatizo ya usingizi, hali inayotajwa kuwa miongoni mwa changamoto kubwa za afya ya akili zinazowaathiri wafanyakazi wengi huku viongozi wengi wa taasisi wakikosa uelewa wa kutosha kuhusu tatizo hilo.
Aidha, alisema mzigo wa mikopo kutoka taasisi za kifedha umeendelea kuwa chanzo kingine cha msongo wa mawazo na changamoto za afya ya akili kwa wafanyakazi na makundi mbalimbali ya jamii.
Ambrose alisema ushirikiano kati ya BMI na TAREWU utasaidia kuongeza uelewa wa masuala ya afya ya akili na kuweka mifumo bora ya kusaidia wafanyakazi kuwa na ustawi unaochochea maendeleo ya mtu mmoja mmoja na taasisi kwa ujumla.
.jpeg)
Mkuugenzi wa BodyMind Insight Dkt.John Ambrose akizungumza namna watavyotoa huduma kwa wanachama wa TAREWU kuhusiana Afya ya Akili na Saikolojia katika maeneo ya kazi

Katibu Mkuu wa Chama cha Wafanyakazi wa Ukusanyaji Mapato Tanzania (TAREWU) Dkt.Michael Marere akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana TAREWU kuingia makubaliano na BodyMind Insight (BMI) kwa ajili ya wanachama wao kupata elimu ya afya ya akili na Saikolojia .
Hati zikioneshwa mara baada ya kusaini makubaliano baina ya Taasisi hizo mbili.
Katibu Mkuu wa Chama cha Wafanyakazi wa Ukusanyaji Mapato Tanzania (TAREWU) Dkt.Michael Marere na Mkurugenzi wa BodyMind Insight (BMI) Dkt.John Ambrose wakisaini hati za makubaliano katika hafla iliyofanyika Ofisi za BMI jijini Dar es Salaam.
Chama cha Wafanyakazi wa Ukusanyaji wa Mapato Tanzania (TAREWU) kimesaini hati ya makubaliano ya ushirikiano wa miaka mitano na kampuni ya BodyMind Insight (BMI) kwa lengo la kuimarisha afya ya akili, ustawi wa kisaikolojia na maendeleo ya wafanyakazi nchini.
Hafla ya utiaji saini wa makubaliano hayo imefanyika katika ofisi za BMI jijini Dar es Salaam, ambapo viongozi wa pande zote mbili walisisitiza umuhimu wa kuweka afya ya akili katika nafasi ya juu ndani ya mazingira ya kazi.
Akizungumza mara baada ya kusaini makubaliano hayo, Katibu Mkuu wa TAREWU, Dkt. Michael Marere, alisema chama hicho kimeamua kuweka kipaumbele katika kulinda afya ya akili na ustawi wa wanachama wake ili kuongeza ufanisi kazini na kuboresha maisha yao kwa ujumla.
Alisema kupitia ushirikiano huo, wanachama wa TAREWU watapata elimu kuhusu afya ya akili, ustawi wa kisaikolojia na mbinu za kukabiliana na changamoto mbalimbali zinazoweza kuathiri utendaji wao wa kazi.
“Makubaliano haya yatadumu kwa kipindi cha miaka mitano na yanaweza kuongezwa baada ya muda huo kuisha kulingana na mafanikio yatakayopatikana,” alisema Dkt. Marere.
Aliongeza kuwa afya ya akili imekuwa suala muhimu katika mazingira ya kazi ya kisasa na inahitaji kupewa uzito sawa na afya ya mwili kutokana na mchango wake katika kuongeza tija na ubunifu kazini.
“Wafanyakazi wenye afya bora ya akili huongeza ufanisi katika utekelezaji wa majukumu yao na kuchangia maendeleo ya taasisi pamoja na taifa kwa ujumla. Katika mazingira ya kazi yanayobadilika kwa kasi, ni muhimu kuwawezesha wafanyakazi kujenga ustahimilivu wa kukabiliana na changamoto za maisha na kazi,” alisema.
Kwa upande wake, Mkurugenzi wa BMI, John Ambrose, alisema afya ya akili ndiyo msingi wa mafanikio ya mtu binafsi na taasisi, akisisitiza umuhimu wa kujenga mazingira salama yanayozingatia ustawi wa wafanyakazi.
Ambrose alisema changamoto za afya ya akili zinaendelea kuongezeka duniani, huku ripoti ya Afya ya Akili Mahali pa Kazi ya mwaka 2026 ikionyesha kuwa asilimia 61 ya wafanyakazi wameongeza matumizi ya likizo zinazohusiana na afya ya akili mwaka huu.
Aliongeza kuwa asilimia 36 ya wafanyakazi duniani wanakabiliwa na matatizo ya usingizi, hali inayotajwa kuwa miongoni mwa changamoto kubwa za afya ya akili zinazowaathiri wafanyakazi wengi huku viongozi wengi wa taasisi wakikosa uelewa wa kutosha kuhusu tatizo hilo.
Aidha, alisema mzigo wa mikopo kutoka taasisi za kifedha umeendelea kuwa chanzo kingine cha msongo wa mawazo na changamoto za afya ya akili kwa wafanyakazi na makundi mbalimbali ya jamii.
Ambrose alisema ushirikiano kati ya BMI na TAREWU utasaidia kuongeza uelewa wa masuala ya afya ya akili na kuweka mifumo bora ya kusaidia wafanyakazi kuwa na ustawi unaochochea maendeleo ya mtu mmoja mmoja na taasisi kwa ujumla.
.jpeg)
Mkuugenzi wa BodyMind Insight Dkt.John Ambrose akizungumza namna watavyotoa huduma kwa wanachama wa TAREWU kuhusiana Afya ya Akili na Saikolojia katika maeneo ya kazi

Katibu Mkuu wa Chama cha Wafanyakazi wa Ukusanyaji Mapato Tanzania (TAREWU) Dkt.Michael Marere akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana TAREWU kuingia makubaliano na BodyMind Insight (BMI) kwa ajili ya wanachama wao kupata elimu ya afya ya akili na Saikolojia .
Hati zikioneshwa mara baada ya kusaini makubaliano baina ya Taasisi hizo mbili.
Katibu Mkuu wa Chama cha Wafanyakazi wa Ukusanyaji Mapato Tanzania (TAREWU) Dkt.Michael Marere na Mkurugenzi wa BodyMind Insight (BMI) Dkt.John Ambrose wakisaini hati za makubaliano katika hafla iliyofanyika Ofisi za BMI jijini Dar es Salaam.

Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...