Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Mauritius, Kamishna wa Polisi (CP) Suzan Kaganda, mwenye makazi yake ya kikazi Jijini Harare, Zimbabwe, amewasilisha Hati za Utambulisho kwa Rais wa Jamhuri ya Mauritius, Mhe. Dharambeer Gokhool, katika hafla iliyofanyika Julai 6, 2026, Ikulu ya Serikali iliyopo Reduit, Mauritius.
Baada ya kuwasilisha hati hizo, Balozi Kaganda alifanya mazungumzo na Mheshimiwa Rais Gokhool, ambaye alimpongeza kwa uteuzi wake na kumkaribisha rasmi katika eneo lake la uwakilishi, huku Rais huyo pia akimhakikishia ushirikiano na Serikali ya Mauritius katika kipindi chote cha utekelezaji wa majukumu yake ya kidiplomasia.
Kwa upande wake, Balozi Kaganda alishukuru kwa mapokezi mazuri aliyopatiwa na kuahidi kuendeleza ushirikiano wa karibu na Serikali ya Mauritius katika kuimarisha uhusiano wa kidiplomasia kati ya Tanzania na Mauritius ambapo aliweka wazi kuwa dhamira yake ni kuendeleza ushirikiano katika sekta za biashara, uwekezaji, utalii na Uchumi wa Buluu kwa manufaa ya wananchi na maendeleo ya nchi hizo mbili.
Balozi (CP) Kaganda pia anaiwakilisha Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Zimbabwe, akiwa na makazi ya kikazi jijini Harare.





.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...