Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam

MIXX imewakutanisha wajasiriamali 18 katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (Sabasaba), ikiwa ni sehemu ya jitihada za kuwawezesha kutangaza bidhaa na huduma zao pamoja na kupanua masoko.


Akizungumza katika maonesho hayo, Mkuu wa Kanda ya Kusini ya Dar es Salaam wa MIXX by YAS, Robert Kasulwa, alisema wajasiriamali hao ni wanufaika wa awamu ya pili ya mradi wa Anzia Ulipo, unaolenga kuwawezesha Watanzania kujikwamua kiuchumi kupitia ujasiriamali.

Kasulwa alisema katika awamu hiyo, jumla ya wajasiriamali 48 wamenufaika na mafunzo pamoja na uwezeshaji wa biashara, huku 18 kati yao wakipata nafasi ya kushiriki maonesho ya Sabasaba ili kutangaza bidhaa zao na kukutana na wateja pamoja na wadau mbalimbali wa biashara.

Alieleza kuwa lengo la mradi huo ni kuwafikia Watanzania wengi zaidi na kuwainua kiuchumi kwa kuwajengea uwezo wa kuanzisha na kukuza biashara endelevu katika maeneo mbalimbali nchini.

"MIXX by YAS inaendelea kushirikiana na wajasiriamali kwa kuwapa fursa za kujifunza, kuonyesha bidhaa zao na kupanua mtandao wa biashara. Tunaamini uwezeshaji huu utachochea ukuaji wa uchumi wa mtu mmoja mmoja na Taifa kwa ujumla," alisema Kasulwa.

Aliongeza kuwa kampuni hiyo itaendelea kutekeleza programu mbalimbali za uwezeshaji wa wananchi kwa lengo la kuongeza ushiriki wa Watanzania katika shughuli za kiuchumi na kutumia huduma za kifedha za kidijitali kukuza biashara zao.



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...