Na Said Mwishehe, Michuzi TV
SERIKALI kwa kushirikiana na Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo (UNDP), Umoja wa Ulaya (EU) na Ubalozi wa Ireland imezindua awamu ya nne ya ufadhili wa masomo ya nishati endelevu kwa wanawake 15 nchini.
Hatua hiyo itafanya idadi ya wanufaika wa mpango wa Women in Sustainable Energy (WISE) kufikia 60 tangu ulipoanzishwa mwaka 2023 kwa ushirikiano kati ya Wizara ya Nishati na Taasisi ya Teknolojia Dar es Salaam (DIT), ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuongeza ushiriki wa wanawake katika sekta ya nishati.
Akizungumza katika uzinduzi wa dirisha la maombi jijini Dar es Salaam, mwakilishi wa Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, Emilian Nyanda, amesema Serikali inawekeza katika maendeleo ya rasilimali watu ili kuhakikisha nchi inakuwa na wataalamu wa kutosha wa kusimamia mabadiliko ya sekta ya nishati.
Amesema Tanzania inaendelea kutekeleza mikakati ya kuongeza uzalishaji wa umeme, kuimarisha matumizi ya nishati jadidifu, matumizi bora ya nishati na ajenda ya nishati safi ya kupikia, lakini mafanikio ya mipango hiyo yanategemea pia upatikanaji wa wataalamu wenye ujuzi.
"Haya si masomo pekee; ni uwekezaji wa moja kwa moja katika wataalamu watakaosimamia sera, teknolojia na ubunifu utakaoiwezesha Tanzania kufikia malengo yake ya maendeleo ya sekta ya nishati," amesema.
Nyanda amesema wahitimu wengi wa awamu tatu zilizopita tayari wamepata ajira katika Wizara ya Nishati, TANESCO, taasisi za utafiti na kampuni binafsi, huku wengine wakianzisha biashara zinazotoa huduma za kitaalamu katika sekta hiyo.
Amefafanua programu hiyo pia inaunga mkono utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, Mkakati wa Nishati Safi ya Kupikia na mpango wa Mission 300 unaolenga kuongeza upatikanaji wa umeme kwa Waafrika milioni 300 ifikapo mwaka 2030.
Kwa upande wake, Meneja wa Maendeleo ya Vipaji wa UNDP Tanzania, Veronica Sigala, amesema mpango wa WISE unalenga kuwawezesha wanawake vijana kupata elimu ya juu na ujuzi wa kitaalamu utakaowawezesha kushiriki kikamilifu katika mabadiliko ya sekta ya nishati.
Amesisitiza mpango huo unachangia utekelezaji wa Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs), ikiwemo elimu bora, usawa wa kijinsia, nishati safi na nafuu, ajira zenye staha na hatua dhidi ya mabadiliko ya tabianchi.
"Tanzania haiwezi kufanikisha mabadiliko ya sekta ya nishati kupitia miundombinu, sera na fedha pekee. Tunahitaji watu wenye ujuzi, na wanawake lazima wawe miongoni mwa wahandisi, watafiti, wabunifu na viongozi wa mabadiliko hayo," amesema.
Kwa upande wake Mkuu wa Taasisi ya Teknolojia Dar es Salaam(DIT), Profesa Preksedis Ndomba, amesema programu hiyo inaendana na maono ya taasisi ya kutumia elimu, utafiti na ubunifu kutatua changamoto za maendeleo ya taifa.
Amesema DIT imeongeza idadi ya wanafunzi wanawake katika taaluma za uhandisi kutoka asilimia 14 mwaka 2016 hadi asilimia 25 kwa sasa, huku ikilenga kufikia asilimia 35 mwaka 2031 na uwiano wa asilimia 50 kwa 50 ifikapo mwaka 2050.
Prof.Ndomba amesema zaidi ya asilimia 60 ya mafunzo yanayotolewa chuoni hapo ni ya vitendo kupitia mfumo wa Teaching Factory, hatua iliyowezesha zaidi ya asilimia 70 ya wahitimu kupata ajira au kujiajiri ndani ya miezi sita baada ya kuhitimu.
Amewahimiza wanawake wenye sifa kutumia fursa hiyo ya ufadhili, akisema kuongeza ushiriki wao katika sekta ya nishati kutasaidia kuimarisha ubunifu, kuongeza nguvu kazi yenye ujuzi na kuharakisha maendeleo ya uchumi wa Tanzania.
SERIKALI kwa kushirikiana na Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo (UNDP), Umoja wa Ulaya (EU) na Ubalozi wa Ireland imezindua awamu ya nne ya ufadhili wa masomo ya nishati endelevu kwa wanawake 15 nchini.
Hatua hiyo itafanya idadi ya wanufaika wa mpango wa Women in Sustainable Energy (WISE) kufikia 60 tangu ulipoanzishwa mwaka 2023 kwa ushirikiano kati ya Wizara ya Nishati na Taasisi ya Teknolojia Dar es Salaam (DIT), ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuongeza ushiriki wa wanawake katika sekta ya nishati.
Akizungumza katika uzinduzi wa dirisha la maombi jijini Dar es Salaam, mwakilishi wa Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, Emilian Nyanda, amesema Serikali inawekeza katika maendeleo ya rasilimali watu ili kuhakikisha nchi inakuwa na wataalamu wa kutosha wa kusimamia mabadiliko ya sekta ya nishati.
Amesema Tanzania inaendelea kutekeleza mikakati ya kuongeza uzalishaji wa umeme, kuimarisha matumizi ya nishati jadidifu, matumizi bora ya nishati na ajenda ya nishati safi ya kupikia, lakini mafanikio ya mipango hiyo yanategemea pia upatikanaji wa wataalamu wenye ujuzi.
"Haya si masomo pekee; ni uwekezaji wa moja kwa moja katika wataalamu watakaosimamia sera, teknolojia na ubunifu utakaoiwezesha Tanzania kufikia malengo yake ya maendeleo ya sekta ya nishati," amesema.
Nyanda amesema wahitimu wengi wa awamu tatu zilizopita tayari wamepata ajira katika Wizara ya Nishati, TANESCO, taasisi za utafiti na kampuni binafsi, huku wengine wakianzisha biashara zinazotoa huduma za kitaalamu katika sekta hiyo.
Amefafanua programu hiyo pia inaunga mkono utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, Mkakati wa Nishati Safi ya Kupikia na mpango wa Mission 300 unaolenga kuongeza upatikanaji wa umeme kwa Waafrika milioni 300 ifikapo mwaka 2030.
Kwa upande wake, Meneja wa Maendeleo ya Vipaji wa UNDP Tanzania, Veronica Sigala, amesema mpango wa WISE unalenga kuwawezesha wanawake vijana kupata elimu ya juu na ujuzi wa kitaalamu utakaowawezesha kushiriki kikamilifu katika mabadiliko ya sekta ya nishati.
Amesisitiza mpango huo unachangia utekelezaji wa Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs), ikiwemo elimu bora, usawa wa kijinsia, nishati safi na nafuu, ajira zenye staha na hatua dhidi ya mabadiliko ya tabianchi.
"Tanzania haiwezi kufanikisha mabadiliko ya sekta ya nishati kupitia miundombinu, sera na fedha pekee. Tunahitaji watu wenye ujuzi, na wanawake lazima wawe miongoni mwa wahandisi, watafiti, wabunifu na viongozi wa mabadiliko hayo," amesema.
Kwa upande wake Mkuu wa Taasisi ya Teknolojia Dar es Salaam(DIT), Profesa Preksedis Ndomba, amesema programu hiyo inaendana na maono ya taasisi ya kutumia elimu, utafiti na ubunifu kutatua changamoto za maendeleo ya taifa.
Amesema DIT imeongeza idadi ya wanafunzi wanawake katika taaluma za uhandisi kutoka asilimia 14 mwaka 2016 hadi asilimia 25 kwa sasa, huku ikilenga kufikia asilimia 35 mwaka 2031 na uwiano wa asilimia 50 kwa 50 ifikapo mwaka 2050.
Prof.Ndomba amesema zaidi ya asilimia 60 ya mafunzo yanayotolewa chuoni hapo ni ya vitendo kupitia mfumo wa Teaching Factory, hatua iliyowezesha zaidi ya asilimia 70 ya wahitimu kupata ajira au kujiajiri ndani ya miezi sita baada ya kuhitimu.
Amewahimiza wanawake wenye sifa kutumia fursa hiyo ya ufadhili, akisema kuongeza ushiriki wao katika sekta ya nishati kutasaidia kuimarisha ubunifu, kuongeza nguvu kazi yenye ujuzi na kuharakisha maendeleo ya uchumi wa Tanzania.





Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...