Victor Masangu,Bagamoyo


Mwenyekiti wa Jumuiya ya ya Wazazi Taifa Ndg. Fadhili Maganya amewasa viongozi wa CCM kuhakikisha kwamba wanavalia njuga na kusimamia ipasavyo suala la mikopo ya asilimia kumi ambayo inatolewa na Halmashauri.

Kauli hiyo ameitoa wakati wa ziara yake ya kikazi Wilaya ya Bagamoyo yenye lengo la kuona uhai wa chama pamoja na kuimarisha jumuiya zake zote sambamba na tenbelea miradi ya maendeleo.

Mwenyekiti huyo amebainisha kwamba kumekuwepo na baadhi changamoto ya utoaji wa fedha ambazo zinatolewa na mfuko wa Tasaf aziwafikii walengwa na zinakwenda kwa watu wengine ambao hawastahili

"Kuna malalamiko mengi ambayo yamekuwa yakitolewa na wananchi kuhusiana na suala la utoaji wa fedha ambazo zinatolewa na mfuko wa Tasaf zinakwenda kwa watu wengine ambao hawahusiki kabisa,"amebainisha Mwenyekiti huyo.

Kadhalika amesema kwamba fedha za asilimia kumi ambazo zinatolewa kwa ajili ya makundi ya vijana,walemavu na wanawake zinatakiwa kutolewa kwa walengwa na sio kupewa watu wengine.

Akiwa katika chuo cha uuguzi na ukunga Mwenyekiti huyo amewahimiza wanafunzi hao kuzingatia maadili pamoja na kuwa wazalendo na nchi yao.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo Shaibu Ndemanga amempongeza Mwenyekiti huyo wa Taifa kwa kufanya ziara hiyo ambayo itaweza kuleta matokeo chanya ya kimaendeleo.

Pia Mkuu huyo wa Wiaya amebainisha kuwa serikali imetenga kiasi cha shilingi bilioni 27 kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbali mbali ya maendeleo ikiwemo ujenzi wa bandari.

Naye Mwenyekiti wa chama cha mapinduzi (CCM) Wilaya ya Bagamoyo Abubakari Mlawa amebainisha kwamba bado kuna changamoto ya migogoro ya ardhi katika baadhi ya maeneo na kwamba wameshaanza kuifanyia kazi.

Mbunge wa Jimbo la Bagamoyo Subira Mgalu ameamua kutoa kiasi cha shilingi milioni 5 kupitia mfuko wa Jimbo kwa ajili ya kuweza kukarabati miundombinu ya majengo pamoja na uzio katika chuo cha uuguzi na ukunga Bagamoyo.

Mwenyekiti wa wazazi Mkoa wa Pwani Jackson KItuka amesema wataendelea kushirikiana na viongozi mbali mbali wa chama na serikali kwa ajili ya kuleta maendeleo.

Ziara ya Mwenyekiti wa Jumuiya ya wazazi ya CCM Taifa imeendelea katika Wilaya ya Bagamoyo ambapo imetembelea miradi mbali mbali ya maendelo ikiwemo chuo cha uuguzi na ukunga,chuo cha kilimo kaole,kiwanda cha kuchakata taka hatarishi pamoja na miradi mbali ikiwemo Hospitali ya Chalinze na sekta ya elimu.



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...