MENEJA wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Mkoa wa Kikodi Ilala Musibu Shabani amesema kuwa TRA imejidhatiti kuhakikisha biashara zinakua kwa kukusanya kodi bila kuziathiri ukuaji biashara hizo.

Shabani ameyasema hayo leo Julai 6 Agosti, 2026 wakati akizungumza na wafanyabiashara wa Mtaa wa Kitonga, Kata ya Msongola iliyopo Ilala jijini Dar es Salaam.

Amesema kuwa biashara ndiyo chanzo kikuu cha kodi ambazo ndiyo mhimili wa maendeleo na kujitegemea kwa taifa hivyo ni jukumu la TRA kuzilinda biashara na kuhakikisha zinakua.

“Biashara na kodi ni muhimu sana kwa maendeleo ya taifa letu. Tunaendelea kuimarisha ukaribu kwa kusikiliza changamoto zenu na kuzitatua ili ulipaji na ukusanyaji wa kodi usiwe kizuizi kwa biashara kustawi,” amesema Shabani.

Aidha, amewasisitiza wafanyabiashara hao kuhakikisha wanatimiza wajibu wao wa kikodi ikiwemo kujisajili na kupata TIN, kufanya makadirio na kulipa kodi stahiki kwa wakati.

Kwa upande wao, wafanyabiashara wameipongeza TRA kwa kutenga siku ya Alhamisi kwa viongozi kusikiliza changamoto za walipakodi moja kwa moja, huku wakisifu ukaribu uliopo sasa baina ya TRA na walipakodi.





Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...