MAONESHO ya uchumi bunifu yanayoenda kwa jina la Mashariki Creative Economy Expo 2026 yanaanza  jijini Dar es Salaam kuanzia kesho tarehe 18 hadi 21 Agosti 2026, yakiwakutanisha wabunifu, wawekezaji, watangazaji, wamiliki wa haki, watunga sera na wabunifu wa teknolojia kwa ajili ya kukuza uchumi wa ubunifu barani Afrika.

Maonesho hayo yaliyoandaliwa na taasisi isiyo ya kiserikali ya  Culture and Development East Africa (CDEA) yanalenga kuifanya sekta ya ubunifu kuwa chanzo cha fursa za biashara na uwekezaji, kupitia matumizi ya haki miliki (IP) katika muziki, filamu, fasihi, sanaa za picha, maudhui ya kidijitali na maeneo mengine.

Expo hiyo pia inalenga kujenga ushirikiano wa kimkakati na majukwaa ya habari na burudani kama Azam Max, ili kukuza simulizi za Afrika Mashariki, kuibua vipaji vipya na kuunganisha wabunifu na masoko mapana ya kikanda na kimataifa.

#MasharikiExpo2026 #UchumiWaUbunifu #CDEA #VipajiAfrika #HakiMiliki #DarEsSalaam #AfrikaMashariki

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...