Serikali ya Tanzania na Ujumbe wa Mabalozi wa Umoja wa Ulaya wamekubaliana kuimarisha ushirikiano katika kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji nchini.
Akiongea baada ya kikao hicho, Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Kitila Mkumbo, amesema pande zote mbili zimejadili hatua zilizofikiwa katika kuboresha masuala ya sheria, kodi, utaratibu na urasimu unaowakabili wawekezaji.
"Kumetokea maendeleo katika kuboresha mazingira ya uwekezaji. Tumejadili pia hatua zaidi za kuchukua ili kuwavutia wawekezaji zaidi kutoka Umoja wa Ulaya kuja kuwekeza hapa Tanzania," amesema Waziri Mkumbo.
Ameongeza kuwa Serikali inatekeleza maelekezo ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuhusu kutoa kipaumbele kwa sekta ya kilimo ili kuongeza thamani ya mazao na kuvutia uwekezaji zaidi katika eneo hilo.
Kwa mujibu wa Waziri Mkumbo, mazungumzo kama haya yamekubaliwa kufanyika kila baada ya miezi sita. Kikao kinachofuata kimepangwa kufanyika tarehe 20 Februari 2027






Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...