Na Mwandishi Wetu. Ubungo, Dar es Salaam

MBEZI. Shule ya Msingi Godiana iliyopo Mtaa wa Mpigi Mgoe, Kata ya Mbezi, Wilaya ya Ubungo, imeadhimisha mahafali yake ya tisa ya kuwapokeza wahitimu wa Darasa la Saba.

Mahafali hayo yalihudhuriwa na viongozi wa Kata ya Mbezi, uongozi wa shule, walimu, wazazi pamoja na wanafunzi.

Akizungumza katika hafla hiyo, Diwani wa Kata ya Mbezi, Mheshimiwa Pius Nyatori, aliipongeza shule hiyo kwa juhudi zake katika kutoa elimu na kuahidi kushirikiana na uongozi wa shule pamoja na wadau kutafuta ufumbuzi wa changamoto zinazoikabili shule hiyo.

Miongoni mwa changamoto hizo ni barabara, umeme na maji, ambazo zinaathiri mazingira ya kujifunzia na shughuli za kila siku za shule.

Nyatori alisema suala la maji ni miongoni mwa changamoto zinazohitaji kufanyiwa kazi, akieleza kuwa atazungumza na wadau na mwekezaji ili kuona namna ya kupata ufumbuzi.

“Tunatambua shida ya maji hapa. Tutaongea na mwekezaji ili tuone jinsi ya kuwekeza, kwa sababu watu wengi wanategemea shule hii,” alisema Nyatori.
Kwa upande wake, mmiliki wa Shule ya Godiana alisema ataendelea kushirikiana na serikali, walimu na wazazi kuhakikisha watoto wanapata elimu katika mazingira bora.
Akizungumza katika hafla hiyo, Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Godiana, Bw. Macmin  Silumbu, alisema shule hiyo imekuwa ikifanya vizuri katika matokeo ya kitaifa na anaamini wahitimu wa mwaka huu watafanya vizuri zaidi.

“Leo tumefanikiwa kuwa na mahafali ya tisa. Ukweli ni Mungu ametujalia. Tuna walimu ambao wameshafundisha na tunaamini watoto wetu wanaenda kufanya vizuri,” alisema Silumbu.

Uongozi wa shule umetoa wito wa kuendelea kushirikiana na Serikali ya Kata ya Mbezi pamoja na wadau mbalimbali ili changamoto za barabara, umeme na maji zipatiwe ufumbuzi na kuwezesha wanafunzi kusoma katika mazingira bora.







 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...