Benki ya NMB imeorodheshwa katika nafasi ya tisa duniani ndani ya Daraja la Sita la benki zenye mali ya kati ya Dola za Marekani bilioni 3 na bilioni 10. NMB ni miongoni mwa benki 500 kutoka nchi 89 zilizojumuishwa katika orodha ya Forbes ya World’s Top Performing Banks 2026.

Forbes na Statista zilifanya tathmini hiyo kwa kuzingatia uwezo wa kupata faida, ukuaji na ubora wa mapato, uimara wa mtaji na vyanzo vya fedha, pamoja na ubora wa mali na ufanisi wa uendeshaji. Mwaka 2025, NMB iliripoti faida baada ya kodi ya takribani Sh760 bilioni na mali ya Sh17.6 trilioni.

Mkurugenzi Mtendaji na Afisa Mtendaji Mkuu wa NMB Bank Plc, Ruth Zaipuna, amesema utambuzi huo unaakisi mageuzi ya muda mrefu ya benki na uwezo wa sekta ya benki Tanzania kushindana kimataifa.

Zaipuna amesema NMB itaendelea kutumia ukubwa wake, teknolojia, ushirikiano na uwezo wa kifedha kupanua upatikanaji wa mitaji katika kilimo, viwanda, biashara, miundombinu na uchumi wa kidijitali, ikiwa ni sehemu ya kusaidia utekelezaji wa Dira 2050.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...